Business
Ali Mbogo Aitaka Pwani Kuwawezesha Vijana Kunufaika na Uchumi wa Baharini
Serikali za kaunti za pwani zimetakiwa kuwawezesha vijana katika masuala ya ubaharia ili kujiendeleza kiuchumi.
Aliyekuwa mbunge wa Kisauni, Ali Mbogo, amesema kuwa ukosefu wa mikakati mwafaka kutoka kwa viongozi kuwawezesha vijana umechangia vijana wengi kukosa vibali muhimu vinavyohitajika ili kuajiriwa katika sekta hiyo ya uchumi wa baharini.
Mbogo ameeleza kuwa Pwani iko na fursa nyingi za kiuchumi kupitia bahari, na ni jambo la kusikitisha kuona vijana wakiachwa nyuma kwa kukosa mafunzo na vyeti vinavyotambulika kimataifa ili kuwawezesha kunufaika na ajira hizo.
Wakati uo huo mwenyekiti huyo wa bodi ya bandari ya LAPSSET amewahimiza vijana ambao hawakubahatika kuendelea na masomo, kujiunga na vyuo vya ufundi ili wapate ujuzi wa kazi za mkono na vyeti vitakavyowawezesha kupata ajira.
“Kuna nafasi nyingi sana katika bandari ya Mombasa lakini tuliowachangua hawatujali bali kujijali wenyewe.”