Sports
Harambee Stars Kuvaa Angola Jioni ya Leo Kusaka Alama Tatu Muhimu CHAN
Timu ya taifa ya soka, Harambee Stars, itashuka dimbani jioni ya leo kuwania alama tatu muhimu dhidi ya Angola, katika mechi yao ya pili ya mashindano ya CHAN kwenye Uwanja wa Kasarani.
Kocha wa Harambee Stars amekiri kuwa haitakuwa mechi rahisi, lakini ana imani kuwa kikosi chake kiko tayari kwa kibarua hicho kigumu.
“Angola walicheza vizuri dhidi ya Morocco. Walikuwa na zaidi ya mashuti 10 golini mwa wapinzani wao, lakini walishindwa kufunga. Niliwaangalia wakicheza — ni timu inayounda nafasi nyingi, hivyo si wapinzani wa kubeza hata kidogo licha ya kupoteza mechi yao ya kwanza,” alisema kocha huyo.
Katika taarifa nyingine, kocha huyo amefichua kuwa mshambulizi Masoud Juma huenda akaukosa mchuano wa leo kufuatia jeraha alilopata kwenye mechi dhidi ya DR Congo. Hali yake bado ni ya mashaka huku akisubiri tathmini ya mwisho kutoka kwa madaktari wa timu.
“Masoud alipata kugongwa dhidi ya DR Congo na kwa sasa hali yake haijaridhisha. Madaktari watatupa taarifa ya mwisho, lakini inaelekea hatacheza mechi ya leo. Kwa upande mwingine, Manzur Suleiman amepona jeraha lake na yuko tayari kuanza mechi hiyo,” aliongeza.
Harambee Stars wanatarajiwa kushuka uwanjani saa moja usiku, kabla ya pambano la awali kati ya Zambia na DR Congo litakalopigwa saa kumi na mbili jioni.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

