Sports
Kikosi Cha Handiboli Ya Ufukweni Yajinoa Tayari Kwa Kombe La Dunia
Katibu Mkuu ambaye pia ni msimamizi wa mchezo wa Handiboli ya Ufukweni (Beach Handball) ya Kitaifa Bi Carolyne Nyadiero amesema kwamba mandalizi yamekamilika kwa ajili ya safari yao ya kuelekea Tunisia wikendi hii.
Akizungumza na Kipenga cha Coco Fm Bi Nyadiero amesema kwamba malengo yao ni kumaliza wa kwanza Barani Afrika na kufuzu Olimpiki Mwaka 2026 kule Dakar Senegal.
“Nataka nishukuru Mungu pili nishukuru gavana wa kaunti hii na washikadhau ikiwemo Rais wa chama cha mchezo huu na waziri wa michezo ambao wametushika mkono tangu tulipopokea barua ya mashindano haya,Lengo letu ni kushinda ubingwa na kushiriki olimpiki 2026 nchini Senegal.
Kwa upande wake kocha wa kikosi cha wanaume Boaz Maroko amesema kwamba mandalizi ya kikosi hicho yamekua mazuri na wanalenga kushinda kombe hilo ama kuwa bora barani afrika.
“Tumejiandaa tangu mwaka jana na vijana wako katika hali shwari tunataka wa kwanza barani afrika kando na kushinda ubingwa wa kombe hili la dunia.”
Ni kauli ambayo imeweza kuungwa mkono na kocha wa kikosi cha akina dada Titus Kasekwa.
“Tumejiandaa vizuri zaidi Makala yaliyopita tulipata silver ila mwaka huu tunataka kupata tuzo kuu na kunyakua dhahabu kwenye mashindano haya.
Kikosi hicho kinakamilisha mazoezi yake siku ya Ijumaa kabila kuondoka Jumamosi kwa kombe la dunia nchini Tunisia.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

