Sports
Palmer apewa jezi namba 10 Chelsea
Kilabu ya Chelsea imetangaza kumpa jezi namba 10 kiungo mbunifu wa kilabu hiyo Cole Palmer raia wa Uingereza baada ya kuonyesha ubora wake tangu kusajiliwa kutoka kilabu ya Manchester City misimu miwili iliopita.
Jezi hilo limekua likivaliwa na mshambulizi wa taifa la Ukraine Mikhael Mudrykambaye amefungiwa kucheza kutokana na tuhuma za utumizi wa dawa za kulevya ama ulaji muuku jambo ambalo huenda limesababisha hatua hiyo kuchukuliwa na uongozi wa The Blues.
Timu Hiyo hata hivyo haijatoa ripoti yoyote kuhusiana na hatima ya mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa kitita cha pauni milioni 89 akitokea Shaktar Donesk ya Ukraine.
Mudryk mwenye umri wa miaka 24 alijiunga na Chelsea mwaka 2023 akifanikiwa kufunga magoli 5 katika mechi 53 ambazo ameshirikisha na kocha Enzo Maresca na hajachezea kilabu hiyo tangu mwaka jana akizidi kuwa gizani kwenye kilabu ya chelsea.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

