Sports
Ureno Mabingwa Uefa Nations Ligi
Timu ya taifa la Ureno ndiyo mabingwa taji la Uefa Nations Ligi baaday ya kucharaza majirani wao Uhispania magoli 5-3 kupitia matuta au Penalti ukipenda
Hii baada ya timu zote kutoshana nguvu magoli 2-2 muda wa kawaida na ule ziada mechi iliopigwa ugani Allianz Arena.
Kiungo anayeiwindwa na Arsenal Martin Zubimendi aliwaweka uongozini The La Furia Rojas kwa faida ya Uhispania kunako dakika ya 21 kabila ya beki matata wa kushoto Nuno Mendes kuishazishia Ureno kunako dakika 26 kipindi cha kwanza.
Mshambulizi wa Real Sociadad Mikel Oyarzabal alirejesha tena mabingwa hao watetezi uongozini kunako dakika ya 45 kabila mshmabulizi nguli na mwamba wa miaka mingi Christiano Ronaldo kusawazishia Ureno dakika 61 kipindi cha pili.
Katika mechi ya kutafuta nafasi ya tatu Ufaransa walinyuka Ujerumani magoli 2-0.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

