News

Auma: Serikali inahusika na visa vya utekaji nyara

Published

on

Afisa wa masuala ya dharura katika Shirika la kutetea haki za kibinadamu la MUHURI Francis Auma alisema serikali kuu inahusika na visa vya utekaji nyara licha ya kujitenga na tetesi hizo.

Auma alidai kwamba serikali kuu inahusika kwa asilimia kubwa katika ukiukaji wa haki za kibinadamu nchini Kenya na inapaswa kuweka wazi suala hilo ili Wananchi wafahamu mahali walipo jamaa zao.

Kulingana na Auma, visa hivyo ambavyo hadi sasa vinaendelea kutekelezwa nchini Kenya vinatekelezwa na serikali kuu.

“Kwa muda mrefu sisi tumepigania masuala haya, watu washikwe, tunataka uwajibikaji na tunataka polisi wawajibike’’, alisema Auma.

Auma pia alipuuzilia mbali msamaha wa Rais William Ruto kwa vijana wa kizazi cha Gen–Z akidai haukuwa wa kweli na ulilenga kuwafumba macho wakenya hasa familia ambazo ziliwapoteza wapendwa wao wakati wa maadamano ya Gen -Z.

Taarifa ya Janet Mumbi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version