Sports
Harambee Stars Yaondoka Kuivaa Chad
Timu ya taifa Harambee Stars kushuka dimbani kucheza na Chad Juni 7,mechi hio ya kirafiki ikipigwa katika ardhi ya morocco kabla ya mechi ya pili juni 10.
Kwa mujibu wa kocha mkuu Benni McCarthy Mechi hizo mbili zitasaidia kikosi hicho kujinoa kwa mashindano ya CHAN mwezi Agosti humu nchini.
“Hizi ni mechi kwa mimi kupata nafasi ya kuwajua vyema wachezaji wangu lakini pia kujiandaa kwa ajili ya taji la Chan kwani hatutaki kuwa tu washiriki bali tunataka kuwa wapinzani pia.”
Kikosi kilichosafiri cha Stars ni pamoja na Magolikipa:
Brian Bwire,Farouk Shikhalo,Sepstanious Wekesa.
Mabeki; Brian Mandela,Alphonce Omija,Sylvester Owino,Siraj Mohammed,Abud Omar,Daniel Sakari,Swale Pamba na Lewis Banda.
Kiungo;Brian Musa,Alpha Onyango,Austine Odhiambo,Ben Stanley Omondi,Bonface Muchiri ,William Lenkupae,Adam Wilson ,James Kinyanjui na David Sakwa.
washambulizi;Beja Nyamawi,Moses Shuma na Emmanuel Osoro
Kiungo Mohammed Bajaber amejiondoa kutokana na jeraha.