News

Usalama na Elimu zavuna kwenye bajeti ya kitaifa

Published

on

Waziri wa Fedha nchini John Mbadi alisoma bajeti ya kitaifa ya mwaka wa Fedha wa 2025/2026 ambayo ni makadirio ya takriban shilingi trilioni 4.23.

Akisoma bajeti hiyo katika majengo ya bunge la kitaifa, Waziri Mbadi alisema mgao wa shilingi trilioni 3.13 ni matumizi ya kawaida ya serikali, shilingi bilioni 693.2 kwa matumizi ya maendeleo na mgao wa shilingi bilioni 474.9 ukitengewa serikali za kaunti.

Katika bajeti hiyo, Waziri Mbadi alipendekeza mgao wa shilingi bilioni 202 kwa idara ya ulinzi nchini, shilingi bilioni 125.7 kwa huduma ya usalama wa kitaifa, shilingi bilioni 51.4 zikitengwa idara ya ujasusi nchini, shilingi bilioni 32.5 kwa idara ya polisi nchini na shilingi bilioni 38.1 kwa idara ya magereza.

Waziri Mbadi alipendekeza mgao wa shilingi bilioni 138.1 kwa sekta ya Afya ili kufanikisha miradi mbalimbali ikiwemo ule wa Afya kwa wote UHC, shilingi bilioni 3.8 kwa masuala ya ardhi nchini huku shilingi bilioni 82.8 kwa sekta ya Kilimo nchini.

Waziri Mbadi, na wabunge katika majengo ya bunge la kitaifa.

Hata hivyo sekta ya elimu nchini ilitengewa mgao wa shilingi bilioni 702.7, ambapo shilingi bilioni 387.2 zimetengwa kuajiri walimu wa CBC, shilingi bilioni 5.9 kusimimia mitihani ya kitaifa, shilingi bilioni 7 kusimamia masomo ya shule za msingi, shilingi bilioni 51.9 kusimamia shule za upili na shilingi bilioni 28.9 kwa sekondari msingi.

Kulingana na Waziri Mbadi, Serikali imepunguza ushuru wa mchele kutoka nje, Wajenzi na wanaofanya kazi za ngozi wamepata afueni huku Mbadi akiongeza ushuru wa bidhaa za Anasa kama vileo Wageni wanaofanya biashara za pesa mtandaoni kulipia

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version