News
Jefwa, Afikishwa Mahakamani kwa Kumjeruhi Mwanamke
Mwanamume mmoja amefikishwa katika Mahakama ya Kilifi kwa kosa la kumpiga na kumjeruhi mwanamke kwa kisingizio cha uchawi.
Mahakama imearifiwa kwamba mnamo tarehe 6 mwezi Disemba mwaka 2024, mshukiwa kwa jina Jefwa Kambengu Leso, alimvamia mlalamishi Dama Mkare Lewa akiwa njiani na kumpiga hadi kumjeruhi.
Mahakama imeelezwa kwamba mshukiwa alimziba pua na mdomo mlalamishi ili kuzuia asipige kelele na kufanikiwa kutekeleza kitendo hicho katika eneo la Mdzongoloni Wadi ya Tezo katika kaunti ya Kilifi.
Hakimu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa, ameagiza mshukiwa wa kesi hiyo kufika Mahakamani mnamo tarehe 14 mwezi Julai mwaka huu pamoja na kuagizwa kusitisha vitisho dhidi ya mlalamishi.