News
Jubilee yaunga mkono maandamano ya kupinga bei ya mafuta
Kufuatia sakata ya uagizaji wa mafuta ghushi nchini, sasa Muungano wa upinzani umetishia kufanya maandamano kuanzia wiki ijayo.
Mwenyekiti wa kitaifa wa Chama cha Jubilee Vincent Kemosi, alisema maandamano hayo yanalenga kushinikiza kupunguzwa kwa bei ya mafuta nchini, akimshtumu Rais William Ruto kwa kuchangia mahangaiko wakenya.
Katika kikao na Wanahabari mjini Kilifi kaunti ya Kilifi baada ya kufanya kifanya kikao na viongozi wa chama hicho kanda ya Pwani, Kemosi aliikosoa serikali, akisema wakenya wamechoka kudanganywa na serikali iliyofeli kutekeleza ahadi zake.
“Serikali imeonyesha kushindwa kutatua suala la mafuta na imeonyesha wazi kwamba imefeli, huezi badilisha ushuru wa mafuta baada ya wananchi kulalamika mbona hakufanya hivyo tangu mwanzo, wakenya wamechoka”, alisema Kemosi.
Kemosi, amepinga mpango wa kugawa maeneo kisiasa yaani Zoning, akisema Viongozi wa Chama cha Jubilee watazingatia haki na usawa pamoja na kuandaa uchaguzi wa mashinani wa viongozi wa chama hicho, kauli iliyoungwa mkono na Mwenyekiti wa chama hicho kaunti ya Kilifi Anthony Kingi.
“Katika ya Kenya haijasema mambo ya Zoning, kila mtu ana haki ya kupigania wadhfa anataka, na sisi kama Chama cha Jubilee hatuingi mkono mambo ya zoning, tutahakikisha uchaguzi unafanyika mashinani kwa haki na uwazi”aliongeza Kemosi.

Viongozi wa Chama cha Jubilee wakiongozwa na Mwenyekiti wa kitaifa wa Chama hicho wafanya mkutano wa kuimarisha chama mashinani, Kilifi
Viongozi hao pia waliwarai wananchi kutathmini viongozi wao na kujiunga na vyama vinavyozingatia haki na usawa, wakisisitiza kuunga mkono upinzani.
Katika swala la raslimali, viongozi hao wameshtumu kutengwa kwa raslimali za Pwani hasa zao la mzani na mkorosho, wakisema wakati umefika kwa mpwani kutambulika na raslimali zake kuthaminiwa.
“Zao la Mnazi na Mkorosho ambayo ndio raslimali ya mpwani imetengwa tangu taifa ipate uhuru ndio sisi tunasema ni lazima raslimali ya mpwani pia nayo itambulike kikamilifu”, alisema Garama.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi.