News

Kaunti ya Kilifi yashindwa kutumia milioni 220 ya bajeti yake

Published

on

Ripoti ya mkaguzi wa bajeti nchini imebaini kwamba kaunti ya Kilifi haijatumia mgao wa bajeti ya shilingi milioni 220 uliotengewa mpango wa kushughulikia athari za mabadiliko ya hewa na tabia nchi katika kaunti ya Kilifi.

Hii ina maana kwamba fedha hizo sasa zitalazimika kurejeshwa kwenye hazina kuu ya taifa kama mojawapo ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa baada ya kaunti kushindwa kutumia fedha ilizotengewa.

Kwa mujibu ya ripoti hiyo, hii sio mara ya kwanza kwa kaunti ya Kilifi kushindwa kutumia mgao wa fedha inayotengewa kwani mnamo 2023 kiasi cha fedha kipatacho milioni 30.6 zilizotengewa miradi ya maendeleo kwa maeneo bunge hazikutumika fedha hizo zikalazimika kurejeshwa kwenye serikali kuu.

Msimamizi wa bajeti, Margaret Nyakang’o alihoji kwamba kwa jumla kaunti ya Kilifi ilifeli kutumia nusu ya bajeti iliyotengewa mwaka 2023- 2024 maswali yakiibuka kuwa ni vipi kaunti ya Kilifi inamudu kustawi kupitia raslimali zinazopaswa kumnufaisha mwanachi wa Kilifi.

Taarifa yake Hamisi Kombe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version