News
Kenya Police Bullets Mabingwa KWPL
Kilabu ya akina dada Kenya Police Bullets ndiyo mabingwa wa ligi ya taifa akina dada kwpl baada ya kuwanyuka Trinity starlets magoli 4-0 mechi ya mwisho hapo jana ugani afraha stadium Nakuru
Winga matata Emily Kemunto moranga alifungua ukurasa wa magoli dkaika 40,kisha Mshambulizi matata Rebecca Becky Okwaro akifunga magoli matatu dakika ya 55 ,dakika ya 79 na dakika 89 na kuchukua kiatu cha dhahabu kwa kufunga magoli 16 msimu huu
Kocha wa Bullets Beldine Odemba hakuficha furaha yake baada ya kushinda kombe hilo kwa mwaka wa pili mfululizo akitaja kwamba upinzani ulikua mkali ila wasichana wake wamepigana mpaka siku ya mwisho kubeba taji hilo.
Katika matokeo mengine
Kisped Queens 2-1 Vihiga Queens
Bunyore Starltes 0-3 Bungoma Queens
Kibera soccer Women 7-0 Mombasa olympic
Ulinzi Starlets 4-0 Kisumu All Starlets
JEDWALI
Bullets alama 46
Ulinzi starlets 45
Kibera soccer alama 42
Kayole starlets ni mabingwa wa KWNSL Baada ya kunyuka kayolets 3-0 madira soccer assasin
Iron ladies 3-0 Diani Quens na kushinda taji la fkf divisheni ya kwanza.