Business
Kenya Yapiga Hatua Kubwa Katika Kuboresha Uchumi wa Bahari na Maziwa – Wadau Wasema
Washikadau katika sekta ya uchumi wa rasilimali za baharini na maziwa katika ukanda wa Pwani wamesema kuwa Kenya imepiga hatua kubwa katika juhudi za kuimarisha sekta hiyo muhimu ya kiuchumi.
Wakizungumza na vyombo vya habari, wadau hao walieleza kuwa serikali imeonyesha dhamira ya dhati ya kuboresha uchumi wa buluu kupitia uwekezaji katika mafunzo ya kitaalamu pamoja na usambazaji wa vifaa vya kisasa vinavyowawezesha wavuvi na wafanyabiashara wa baharini kuendeleza shughuli zao kwa ufanisi zaidi.
Aidha, washikadau hao wameitaka serikali kupitia idara husika kuwawezesha vijana zaidi kushiriki kikamilifu katika sekta ya uchumi wa bahari, wakisisitiza kuwa kundi hilo lina mchango mkubwa katika ukuaji endelevu wa sekta hiyo.
Wakati huohuo, wameitaka serikali kuongeza uwekezaji katika sekta ya uchumi wa buluu ili kuimarisha maisha ya jamii zinazotegemea bahari na maziwa kwa riziki.