News
Mahakama yasitisha ujenzi wa kanisa katika Ikulu ya Rais
Mahakama imesitisha ujenzi wowote wa kanisa la kudumu au hata maeneo ya ibada unaoweza kuendeshwa katika ikulu ya rais kwa sasa.
Mahakama pia ilisitisha ujenzi wa maeneo haya ya ibada kwenye ikulu ndogo zote nchini.
Jaji Chacha Mwita alitoa uamuzi huo kufuatia kesi iliyowasilishwa na mashirika ya kutetea haki za binaadam, ikiibua maswali kuhusu sheria, dini na majukumu ya serikali.
Walalamishi kwenye kesi hiyo walisema kuanzishwa kwa miundo mbinu ya kidini kwenye maeneo ya umma kama ikulu, kunaashiria ukiukaji mkubwa wa katiba.
Hatua ya kujengwa kwa kanisa katika ikulu ya rais iliibua hisia mseto nchini huku baadhi ya wananchi na viongizo wa dini wakipinga hatua hiyo.
Walidai hatua hiyo inaenda kinyume na sheria za taifa.
Kesi hiyo itatajwa tarehe 18 Novemba mwaka wa 2025.
Taarifa ya Joseph Jira