News
Mashirika ya kijamii yaelimisha umma kuhusu athari za mazingira
Mashirika mbalimbali ya kijamii kaunti ya Kilifi yanayojihusisha na masuala ya uchumi wa bahari yamejitokeza na kuhamasisha jamii kuhusu athari za mabadiliko ya hali ya anga.
Mpango huo unaoendelezwa na mataifa 5 barani Afrika ikiwemo Kenya, Comoros, Madagascar, Tanzania na Msumbiji, unalenga kudhibiti athari za mabadiliko ya hali ya anga, ambapo nchini Kenya maeneo ya Magarini, Malindi na Kilifi kaskazini unaendelezwa.
Mashirika hayo yakiongozwa na Shirika la Mission Inclusion na Groots Kenya yalifichua kwamba ongezeko la viwango vya chumvi baharini vimechangia pakubwa kushughudiwa kwa idadi ndogo ya samaki baharini.

Wadau wa masuala ya uchumi wa bahari wakongamana Watamu
Hata hivyo wakaazi waliohudhuria Kongamano hilo walishauriwa kuendeleza upanzi wa mikoko katika maeneo ya bahari kama njia mojawapo ya kudhibiti mazingira ya bahari.
Mpango huo ulioanzishwa mwezi Mei mwaka wa 2023 unalenga kuwafikia watu elfu 85 kwa kipindi cha miaka 3.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi