News

Mshukiwa wa kesi ya ulanguzi wa dawa za kulevya kuzuiliwa rumande

Published

on

Mahakama ya Kilifi iliagiza mshukiwa wa kesi ya ulanguzi wa dawa za kulevya kuzuiliwa rumande.

Hii ni baada ya mshukiwa wa kesi hiyo Hamisi Kazungu Ali kushindwa kutoa dhamana ya shilingi laki moja na mdhamini wa kiasi sawa na hicho ama pesa taslimu shilingi elfu 50 wakati uchunguzi wa kesi hiyo ukiendelea.

Akitoa agizo hilo siku ya Jumanne, Septemba 2, 2025, Hakimu wa Mahakama ya Kilifi James Mwaniki amesema mshukiwa kukana mashtaka dhidi yake.

Awali Mahakama ilielezwa kwamba mnamo tarehe 1 mwezi Septemba, 2025 katika eneo la Kibaoni mjini Kilifi masaa ya saa tano asubuhi mshukiwa alipatikana na maafisa wa poliosi wakiwa katika ziara yao ya kiusalama ambapo walimtia nguvuni mshukiwa akiwa na pakti 10 za dawa ya kulevya inayokisiwa kuwa Heroini.

Mahakama hiyo ya Kilifi pia ilisema mshukiwa Hamisi Kazungu Ali anafaa kurejeshwa Mahakamani mnamo tarehe 26 mwezi Septemba, 2025 mbele ya Hakimu Ivy Wasike ambapo kesi hiyo itaendelea.

Taarifa ya Tecla Yeri

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version