News

Murkomen: serikali itaongozwa na usalama wa kitaifa, sio amri za mahakama.

Published

on

Mamlaka ya mawasiliano nchini CA imeondoa amri ya kuzuia vituo vya redio na televisheni kuweka mubashara matangazo kuhusu maandamano.

Uamuzi huo ni kufuatia amri ya mahakama iliyokosoa hatua ya mamlaka hiyo mbali na kuzima mawimbi ya vituo vya runinga tatu za televisheni nchini.

Hata hivyo waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen alisema serikali itaongozwa na usalama wa kitaifa na wala sio amri za mahakama akiongeza kuwa hajutii uamuzi wa kuzima mawimbi ya vituo hivyo.

CA ilitangaza uamuzi huo kufuatia amri ya mahakama iliyotolewa na majaji wawili John Chigiti na Chacha Mwita kufuatia ombi lililowasilishwa mahakamani na shirika la katiba institute, na tume ya kitaifa ya haki za binadam vile vile chama cha mawakili LSK.

Kulingana na Murkomen Vyombo vya habari vilisaidia kuwachochea waandamanaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version