News

Oburu, Awakosoa Wanaopinga Ushirikiano wa Rais Ruto na Raila

Published

on

Seneta wa kaunti ya Siaya, Oburu Oginga amejitokeza na kutetea ushirikiano wa utendakazi kati ya Rais William Ruto na Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga, akisema umeunganisha sehemu ya upinzani na serikali.

Oburu amebainishwa kwamba ushirikiano huo utasaidia kufanikisha utoaji wa huduma bora kwa wakenya wote na haufai kukosolewa.

Oburu amesema viongozi ambao wanaandaa uvumi dhidi ya mpango huo wa ushirikiano wa utendakazi wana malengo mabaya ya kusambaratisha maendeleo, akiwataka kuruhusu eneo la Nyanza kunufaika kimaendeleo.

Kwa upande wake Kiongozi wa walio wachache katika bunge la kitaifa na ambaye pia ni mbunge wa Suna Mashariki Junet Mohammed amewasuta wale wanaopinga ushirikiano huo, akiwataka kupeyana nafasi kwa wakenya kunufaika kimaendeleo.

Hata hivyo Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandayi ameweka wazi kwamba eneo la Nyanza litaendelea kuunga mkono serikali ya Kenya kwanza kwa manufaa ya wananchi wote.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version