Business
Sekta ya biashara yaimarika kaunti ya Homabay
Sekta ya biashara katika kaunti ya Homabay ambako kongamano na ugatuzi linaendelea, imeimarika hata zaidi.
Kulingana na wamiliki wa mikahawa na baa eneo hilo walisema kuwa vyumba vya kukodi vilijaa kutokana na idadi kubwa ya wageni ambao walishiriki kongamno hilo kufanya uchumi wa eneo hilo kuinuka hata zaidi.
Wakizungumza na Mwanahabari wetu ambaye anaendelea kukita kambi katika eneo hilo wamiliki hao wanasema kuwa kwa sasa pesa inazunguka kwa wingi hali ambayo imefanya uchumi kuinuka.
Aidha walisema kuwa kaunti hiyo na wageni ambao wanafanya biashara katika eneo hilo wamenufaika hata zaidi kufuatia ujio wa kongamano hilo.
Waliitaka serikali kuu na kaunti kuendelea kuekeza zaidi kwa vijana kwani wako katika nafasi nzuri ya kuinuka kiuchumi.
Taarifa ya Pauline Mwango