News

Serikali yabaini ulaghai uliofanywa katika NHIF

Published

on

Wizara ya Afya nchini imedai kuwa kumekuwepo na ulaghai mkubwa katika mfumo wa zamani wa bima ya afya ya NHIF.

Waziri wa Afya, Aden Duale alisema kuwa zaidi ya visa milioni 3 vya ada hewa ya matibabu, vimebainika wakati wa shughuli ya uhamisho wa huduma kwenda kwa bima ya afya ya jamii kwa wote (SHA).

Waziri Duale, alidokeza kuwa uchunguzi unaendelea ili kuwatambua wahusika wa sakata hiyo na kuwachukulia hatua kali za kisheria.

Akizungumza mbele ya kamati ya bunge la kitaifa kuhusu afya, waziri Duale alifichua kuwa kuna madai ya udanganyifu unaotekelezwa na baadhi ya hospitali zinazolenga kufyonza fedha kwa njia isiyo halali kutoka kwa bima ya SHA.

Duale aalisema kuna ushahidi kuwa baadhi ya hospitali hudai kutekeleza upasuaji ambao haukufanyika, na hata kuwasilisha madai ya uongo kuhusu watu waliolazimishwa kutoa damu bila sababu za kiafya.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version