News

Spika Kingi aagiza uchunguzi wa haraka kufuatia kifo cha wakili, Nairobi

Published

on

Spika wa bunge la seneti Amason Kingi ameagiza asasi za usalama kufanya uchunguzi wa haraka kufuatia kifo cha wakili mmoja jijini Nairobi Mathew Kyalo Mbobu.

Kingi alitaja mauaji ya wakili huyo kama yakinyama huku akimtaja wakili Mbobu kama mtu jasiri na aliyejitolea kuhudumia raia.

Wakili huyo alifariki baada ya kupigwa risasi jana jioni akiwa katika gari lake kwenye barabara ya Lang’ata.

Taarifa za polisi zilisema mwathiriwa alipigwa risasi na watu waliokuwa kwenye pikipiki muda mfupi baada ya saa moja na nusu usiku.

Ilisemekana wakili huyo alikuwa akiendesha gari kuelekea nyumbani wakati mshambuliaji aliposimamisha pikipiki kando ya gari lake na kufyatua risasi kabla ya kuondoka kwa kasi.

Taarifa ya Joseph Jira.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version