Business

Viongozi wa Mombasa Waisihi Serikali Kuu Kuwekeza Zaidi Katika Uchumi wa Samawati

Published

on

Viongozi wa kaunti ya Mombasa wameitaka serikali kuu kuongeza uwekezaji katika sekta ya uchumi wa raslimali za baharini na maziwa, ili kuinua maisha ya wakazi wa Pwani na kuchangia katika kukuza pato la taifa.

Wakiongozwa na Seneta maalum Miraj Abdillah, viongozi hao wameeleza kuwa ipo haja ya haraka ya kuanzishwa kwa chuo cha mafunzo ya ubaharia katika eneo la Pwani, hatua itakayowawezesha vijana kupata ujuzi muhimu na fursa za ajira katika sekta ya baharini.

Akizungumza na wanahabari, Seneta Miraj alisema kuwa licha ya Pwani kuwa na raslimali nyingi za bahari, vijana wengi bado wanakabiliwa na ukosefu wa ajira na kutokuwa na nafasi ya kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya kiuchumi ya eneo hilo.

Viongozi hao pia wameitaka serikali ya kaunti ya Mombasa kuhakikisha kuwa wavuvi wanapatiwa vifaa vya kisasa, ili kuongeza ufanisi na tija katika shughuli zao za kila siku za uvuvi.

Kwa pamoja, walisisitiza kuwa sekta ya uchumi wa buluu ina uwezo mkubwa wa kubadilisha maisha ya watu wa Pwani, iwapo itawekewa vipaumbele vya kimkakati na uwekezaji wa kutosha kutoka kwa serikali zote mbili—kaunti na taifa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version