News
Viongozi wahofia kulegea kwa kasi ya ujenzi wa barabara, Jaribuni
Viongozi wa kijamii katika eneo la Jaribuni kaunti ya Kilifi wamekashifu vikali hatua ya kufunguliwa kwa barabaraza kuelekea katika timbo za mawe katika eneo la Jaribuni ili kuwawezesha wawekezaji kuendelea na shughuli zao.
Wakiongozwa na Emmanuel Chai maarufu Bwenyenye viongozi hao walisema kuwa huenda ujenzi wa barabara ya Dzitsoni–Jaribuni ukachukua muda mrefu zaidi kutokana na suala hilo.
“Hali ikiendelea jinsi ilivyo basi tutaanzisha mchakato wa kutaka kusimamishwa kwa shughuli za timboni hadi pale ujenzi wa barabara utakapotamatika”, alisema Emmanuel.
Naye Mwenyekiti wa baraza la Wazee wa jamii ya Kauma Samson Mwakudza amepongeza juhudi za wakaazi na viongozi kuwashinikiza wawekezaji kujenga barabara hiyo ya takriban kilomita 14 ambayo imewafaidisha kwa kiwango kikubwa.
Hata hivyo aliwataka wakaazi kushirikiana na mkandarasi wa barabara hiyo ili kufanikisha kukamilika kwa barabara hiyo kwa wakati.
Taarifa ya Hamis Kombe