Business

Wadau wa sekta ya uvuvi walalamikia unyakuzi wa ardhi

Published

on

Kamati ya bunge la kitaifa kuhusu uchumi wa bahari na masuala ya ubaharia imewataka wawekezaji wote waliovamia ardhi zilizotengewa

Kauli hii ilijiri baada ya wavuvi na wasimamizi wa fuo za bahari kuelekeza lalama zao kwa kamati hiyo wakidai kuhangaishwa kila mara na baadhi ya mabwenyenye wanaodaiwa kushirikiana na baadhi ya maafisa wa serikali.

Walidai kwamba unyakuzi huo umekuwa donda sugu na uliadhiri pakubwa shughuli za uvuvi huku wakiitaka serikali ya kitaifa kuingilia kati na kuhakikisha ardhi hizo zinarudhishwa mikononi mwa jamii za wavuvi haraka iwezekanavyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati hiyo na ambaye pia ni mbunge wa Marakwet Mashariki David Kangogo Bowen alisema ujenzi wa kibinafsi katika maeneo ya mita 60 kutoka ukingo wa bahari ni ukiukaji wa sheria kwani maeneo hayo yametengwa mahususi kwa matumizi ya wavuvi.

“Wale wamejenga mita 60 kando ya bahari waondolewa ndio hawa wavuvi wapewe nafasi ya kufanya biashara yao vizuri na pia wapate sehemu ya kuegeza maboti yao”. … alisisitiza David Bowen.

Kauli yake iliungwa mkono na mbunge wa Matunga Kassim Sawa Tandaza aliyesema agizo hilo ni sharti litekelezwa mara moja na yeyote atakayekiuka agizo hilo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version