Sports

Wakenya Timothy na Reynold Cheruiyot wafuzu kwa fainali ya mita 1500, Tokyo

Published

on

Bingwa wa Dunia wa mita 1500 mwaka 2019 Timothy Cheruiyot na bingwa wa dunia kwa chipukizi chini ya umri wa miaka 20 Reynold Cheruiyot wamejikatia tiketi kwa fainali ya mashindano ya Riadha Uimwenguni jijini Tokyo, Japani.

Cheruiyot alifuzu kwa fainali baada ya kumaliza wa nne katika nusu fainali ya kwanza  leo Jumatatu akitimka kwa muda wa dakika 3 sekunde 35 .61.

Upande wake, Reynold aliongoza mchujo wa pili kwa muda wa dakika 3 sekunde 36.64 na kufuzu kwa fainali ya Jumatano.

Mkenya mwingine, Wiseman Were alifuzu kwa nusu fainali ya mita 400 kuruka viunzi.

mbio hizo zinaingia siku ya nne mjini Tokyo Japan .

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version