News
Wakenya waonywa dhidi ya kuchipuka kwa magonjwa msimu wa mvua
Wizara ya Afya nchini imewarai wakenya kuchukua tahadhari ya mapema msimu huu wa mvua na kutibu maji wanayotumia kila siku ili kuepuka kukumbwa na magonjwa mbalimbali.
Katibu katika Idara hiyo Mary Muthoni, alisema baadhi ya maeneo yanashuhudia mvua nyingi na huenda ikaathiri wananchi iwapo hawatakuwa maniki dhidi ya kujikinga na magonjwa.
Alisema mara nyingi magonjwa wengine huchangiwa na mazingira machafu, na maji yaliochanganyika na maji taka, akisisitiza haja ya wananchi kuwa makini na kuhakikisha wanachamsha maji ya kunywa kwa usalama wao.
Katibu huyo alisema watu wengi wamekuwa na hulka ya kutumia maji ya visima na mabwawa na mara nyingi huwa na chembechembe ya viini, akisisitiza haja ya wananchi kuchukua tahadhari ya kutibu maji ama kuchemsha maji ya kunywa kabla ya kuyatumia ili kuepuka maambukizi ya maradhi mbalimbali.
Akizungumza katika kaunti ya Nyeri, Muthoni aliwarai wananchi kutopuuza tahadhari hiyo na kuhakikisha wanalinda afya zao.
“Kuna athari ya kuchupuka kwa magonjwa mbalimbali kama yale ya kuendesha kutokana na uchafuzi wa mazingira na utumizi wa maji ambayo hajatibiwa ama kuchemshwa, kwa hivyo langu ni kuwahimiza wananchi wachukue tahadhari ya mapema hasa msimu huu wa mvua ili kuepuka magonjwa”, alisema Muthoni.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi