Business

Wanawake Pwani Wataka Ushirikishwaji Zaidi Katika Uchumi wa Majini

Published

on

Wanawake kutoka maeneo ya Pwani wanaitaka serikali kuu na zile za kaunti kuhakikisha wanashirikishwa kikamilifu katika sekta ya uchumi wa majini ili kujiendeleza kimaisha.

Wakiongozwa na Mercy Mghanga, wanawake hao wamesema licha ya wanawake wengi kujihusisha na uvuvi na shughuli nyingine za baharini, bado wanakosa vifaa na msaada wa kukuza biashara zao.

Kwa upande wake Linda Shuma wa shirika la Women and Girls Empowerment CBO, amesema kuna haja ya wanawake kushiriki katika michezo ya majini, utalii na usafiri wa baharini ili kuchangia katika ukuaji wa uchumi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version