News

Wazazi walalamikia mazingira duni ya Elimu, Magarini

Published

on

Wazazi katika shule ya msingi ya Tangai eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi wanaiomba serikali pamoja na wahisani kubuni mikakati ya kuboresha miundomsingi ya taasisi hiyo ya elimu hasa majengo ya shule.

Wazazi hao wakiongozwa na Thomas Kombe, walisema baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo hulazimika kuhamia shule nyingine punde wanapofika gredi ya kwanza kutokana na uhaba wa madarasa.

Kombe ambaye pia ni kiongozi wa vijana eneo hilo alilitaja suala la uhaba wa walimu shuleni kama changamoto, akisema shule hiyo ina mwalimu mmoja pekee na madarasa mawili.

“Shule iko lakini ni ndogo hakuna gredi ya kwanza na ya pili hawaweze kutoka Tangai hadi Shaurimoyo na kuna baridi ambayo inafanya watoto wanadhohofika kiafya. Tunaiomba serikali na wahisani watusaidie kuboresha shule yetu”, alisema Kombe.

Wakati uo huo aliiomba serikali kujenga madarasa zaidi katika shule hiyo sambamba na kuongezwa kwa idadi ya walimu kama njia mojawapo ya kuboresha mazingira ya masomo kwa wanafunzi wa shule hiyo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version