News
Waziri Wandayi asema hatajiuzulu
Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandayi ameweka wazi kwamba hatajiuzulu licha ya shinikizo kutoka kwa baadhi ya viongozi wa kisiasa na mashirika ya kijamii, kumtaka ajiuzulu.
Wandayi alisema haoni sababu za kuchukua uamuzi huo kwani hausiki kivyovyote na sakata ya uagizaji wa mafuta ghushi, akisema uchunguzi unaendelea kuhusu suala hilo.
Akijubu maswali yalioulizwa na wabunge mbele ya kamati ya Kawi katika bunge la kitaifa, inayoongozwa na David Gikaria, Waziri hiyo alisema hadi kufikia sasa hajajua kiini kilichowashinikiza maafisa watatu katika wizara yake waliohusisha na sakata hiyo kujiuzulu.
Wandayi alithibitisha kwamba Idara ya Mafuta chini ya Wizara ya Kawi nchini iliomba msamaha wa vigezo fulani kutoka kwa Shirika la ukadiriaji wa bidhaa nchini (KEBS) kupitia barua za tarehe 26 na 27 Machi 2026. Msamaha huo ulitolewa baadaye na Wizara ya Biashara na Viwanda nchini inayoongozwa na Lee Kinyanjui kuridhinia msamaha huo tarehe 28 Machi 2026.
Aidha alifichua kwamba Kamati ya uratibu wa Meli (VAC) ilibaini mnamo tarehe 18 Machi 2026 kuwa meli iliyokuwa imepangwa ilikuwa imepakia mizigo katika bandari ya Jebel Ali lakini haikuweza kupita katika Mlango wa Bahari wa Hormuz, hali iliyozua hofu ya uwezekano wa pengo la usambazaji wa mafuta.
Ilibainika kwamba kauli ya mashirika mbalimbali iliyopendekeza mzigo wa dharura uliwasilishwa kwa Katibu wa Wizxara ya Kawi na mafuta nchini Mohammed Liban kuidhinisha.
Waziri Wandayi hata hivyo alipoulizwa ni wapi hasa usambazaji wa mafuta ulikwama, aliwaelekeza wabunge kwa taratibu za ndani za Kampuni ya usambazaji mafuta (KPC), akisema kuwa kampuni hiyo ilipokea ripoti ya bandari ya kupakia mizigo tarehe 27 Machi ili kuhakikisha inazingatia viwango vinavyohitajika.
Wakati huo huo alidokeza kwamba hakuna na ufahamu kwamba sakata hiyo ilikuwa kinyume na mpango wa uagizaji wa mafuta wa serikali kwa serikali yani G to G, akisema hatua hiyo ndio iliyopelekea kuanzishwa kwa ucnguzi na maafisa wa DCI.