Business
Bei ya mafuta ya Petroli, Dizeli na Taa yapanda
Huenda wakenya wakagharamika zaidi katika kumudu gharama ya maisha kutokana na ongezeko la bei ya mafuta ya Petroli, Dizeli na Taa mtawalia.
Hii ni kutokana na bei mpya iliyotolewa na Mamlaka ya kudhibiti Kawi na mafuta ya Petroli nchini EPRA kwani bei ya mafuta ya Petroli imeongezeka kwa shilingi 8.99, mafuta ya Dizeli kwa shilingi 8.67 na mafuta ya taa kwa shilingi 9.55 kwa lita.
Kulingana na EPRA, bei hiyo mpya itatumika kwa kipindi cha mwezi mmoja hadi Agosti 14, ambapo bei ya mafuta ya Petroli katika jiji la Nairobi itauzwa kwa shilingi 186.31, Diseli kwa shilingi 171.58 na mafuta ya taa kwa shilingi 156.58.
Katika jiji la Mombasa bei hiyo mpya ya mafuta itauzwa kwa shilingi 183.02, mafuta ya Dizeli yatauzwa kwa shilingi 168.30 na mafuta ya taa yatauzwa kwa shilingi 153.29 kwa lita katika kipindi cha siku 30.
Hata hivyo katika kaunti ya Kilifi bei hiyo ya mafuta iko tafauti kwa sasa mafuta ya Petroli yatauzwa kwa shilingi 183.88, mafuta ya Dizeli yakiuzwa kwa shilingi 169.16 na matufa ya taa yatauzwa kwa shilingi 153.29 kwa lita.
Kulingana na taarifa kutoka EPRA, bei hiyo mpya mafuta imetoka na kupanda kwa bei ya mali ghafi kwa asilimia 6.45 ambayo ni Dola za Marekani 590.24 kwa “Cubic metre” kwenye mafuta ya Petroli mwezi Mei mwaka huu.
Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka hiyo Daniel Bargoria alisema japo bei hiyo huenda ikashuka iwapo soko huru la mafuta litapunguza bei ya mali ghafi ambayo imechangiwa na mizozo ya kivita katika mataifa yanayopigana ambayo na yamekuwa yanazalisha mafuta.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi