Sports

Diani Stars na Mwanambeyu Girls washinda mashindano ya kwanza ya soka ya ufukweni ya FKF Kaunti ya Kwale 

Published

on

Kilabu ya Diani Stars walitwaa ubingwa wa wanaume baada ya kuichapa Barbados 4-2, huku Mwanambeyu Girls wakinyakua taji la wanawake kwa ushindi wa 4-2 dhidi ya Diani Queens.

Rais wa Shirikisho la Soka Kenya (FKF), Hussein Mohammed, alisema shirikisho litaendelea kuunga mkono kandanda ya mashinani ili kukuza vipaji zaidi miongoni mwa vijana. Aliongeza kuwa watawekeza kwenye soka ya ufukweni ili kukuza utalii wa michezo, huku akiwataka wawekezaji zaidi kuungana na kushirikiana katika kuandaa mashindano mengi zaidi.

Mashindano hayo, ambayo yalianza mwezi Mei yakichezewa ufukwe wa Kongo mjini Diani, yalihusisha jumla ya timu 24 — timu 16 za wanaume na 8 za wanawake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version