News
IEBC: Vijana wanaitisha pesa kusajiliwa kuwa wapiga kura
Wakenya wanaojitokeza kujisajili kama wapiga kura katika zoezi endelevu lililoidhinishwa na Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC, inatia matumaini ya Tume hiyo kufikia malengo yake ya kusajili wa idadi ya watu milioni 6.2 kote nchini.
Katika kaunti ya Kilifi kwenye eneo bunge la Kilifi Kazkazini ambapo zoezi hilo linaendelea, Maafisa wa Tume hiyo wamedai kupitia changamoto wakati wa usajali wa wapiga kura.
Maafisa hao wanasema kati ya changamoto hizo ni pamoja na kuitishwa pesa na vijana ndipo wawasajili kuwa wapiga kura, wakisema changamoto hiyo inarudisha nyuma juhudi zilizoidhinisha na Tume ya IEBC.
Afisa anayesimamia Tume ya IEBC katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini John Mwawasi alisema licha ya changamoto hizo, kufikia sasa maafisa wa tume hiyo wanaozuru nyanjani wamefanikiwa kusajili wapiga kura wapya kwa asilimia 50.