Connect with us

News

IEBC: Vijana wanaitisha pesa kusajiliwa kuwa wapiga kura

Published

on

Wakenya wanaojitokeza kujisajili kama wapiga kura katika zoezi endelevu lililoidhinishwa na Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC, inatia matumaini ya Tume hiyo kufikia malengo yake ya kusajili wa idadi ya watu milioni 6.2 kote nchini.

Katika kaunti ya Kilifi kwenye eneo bunge la Kilifi Kazkazini ambapo zoezi hilo linaendelea, Maafisa wa Tume hiyo wamedai kupitia changamoto wakati wa usajali wa wapiga kura.

Maafisa hao wanasema kati ya changamoto hizo ni pamoja na kuitishwa pesa na vijana ndipo wawasajili kuwa wapiga kura, wakisema changamoto hiyo inarudisha nyuma juhudi zilizoidhinisha na Tume ya IEBC.

Afisa anayesimamia Tume ya IEBC katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini John Mwawasi alisema licha ya changamoto hizo, kufikia sasa maafisa wa tume hiyo wanaozuru nyanjani wamefanikiwa kusajili wapiga kura wapya kwa asilimia 50.

Mwawasi alisema japo wanalenga kusajili idadi ya wakenya zaidi ya elfu 13 katika eneo bunge hilo, kufikia sasa wamesajili wakenya zaidi ya elfu 6.
“Changamoto ambayo tunapitia kwa sasa ni vijana ambao tunalenga kuwasajili wamekuwa wakiitisha pesa maafisa wetu ili wasajiliwe kuwa wapiga kura wapya lakini tumekuwa tukiwaeleza kwamba zoezi hili ni hiari na kwamba litawapa nafasi nzuri ya kufanya mabadiliko ya kiuongozi kuanzia ngazi ya kitaifa hadi mashinani”,alisema Mwawasi.
Wakaazi waliokuwa wamefika katika ofisi za IEBC kusajiliwa wameelezea wepesi wa zoezi hilo, kutokana na maafisa hao wanatumia mfumo wa kieletronic.
Tume hiyo ya IEBC imejitenga na masuala ya kujihusisha na siasa na kuwarai wanasiasa kuwasaidia katika kuwarai wananchi hasa vijana kujisajili kama wapiga kura, kauli ambayo imeungwa mkono na Naibu Mwenyekiti wa IEBC Fahima Araphat.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending