News
Jackson Chiwai ahukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani
Mahakama ya Kilifi imemhukumu kifungo cha miaka 15 gerezani Jackson Chiwai baada ya Mahakama kumpata na hatia ya kumnajisi mtoto mdogo wa umri wa miaka 5.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa baada ya ushahidi kamili kuwasilishwa Mahakamani.
Hakimu Obulutsa alisema kwamba hukumu hiyo imezingatia ushahidi wote uliyowasilishwa Mahakamani kiwemo ripoti ya daktari kuhusu uchunguzi wa unajisi dhidi ya mtoto huyo.
Kabla ya hukumu hiyo kutolewa, upande wa mashtaka ukiongozwa na Kiongozi wa mashtaka ya umma katika Mahakama hiyo Ridhwan Mohammed ulieleza Mahakama kwamba mnamo tarehe 11 mwezi Mei mwaka 2024 mwendo wa saa moja jioni Jackson alimnajisi mtoto wa miaka 5 ambaye ni binamu yake.
Japo ushahidi wa mlalamishi na mashahidi wengine ambao ni watoto wenzake uliashiria kitendo hicho cha unajisi kuwa kweli baada ya watoto hao kueleza Mahakama kwamba walikuwa wakiangalia runinga chumbani wakati mama yao akiwa jikoni akipika, ambapo Jackson ambaye ni binamu yao aliingia chumbani humo na kumchukua mtoto huyo na kutoka naye nje ambapo alitekeleza kitendo hicho.
Kulingana na ushahidi wa daktari, uchunguzi na vipimo kwa mtoto huyo ilionyesha kwamba mtoto hakuwa amenajisiwa bali kulikuwa na jaribio la dhulma ya kingono kutokana na mikwaruzo kwenye uke wa mtoto huyo.
Uchunguzi wa daktari ulichangia pakubwa kwenye hukumu hiyo ambayo Hakimu Obulusta alieleza kwamba Jackson angehukumiwa kifungo cha maisha kulingana na sheria na uzito wa kesi hiyo.
Mshukiwa alihukumiwa kwa kosa mbadala la kujaribu kumnajisi mtoto huyo na kupata kifungo hicho cha miaka 15.
Mahakama hata hivyo imempa mshtakiwa siku 14 za kukata rufaa iwapo hajaridhishwa na uamuzi wa Mahakama.
Taarifa ya Teclar Yeri.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

