Connect with us

Business

Serikali yachukua hatua za haraka kupunguza bei za mafuta

Published

on

Mamlaka ya kudhibiti bei ya mafuta nchini EPRA imetangaza kupunguzwa kwa bei ya mafuta ya Petroli, Dizeli na Taa humu nchini.

Kaimu Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka hiyo Mhandisi Joseph Oketch katika taarifa aliyoitoa, ametangaza kupunguzwa kwa bei ya mafuta ya petroli kwa shilngi 9.37, mafuta ya Dizeli kwa shilingi 10.21 huku bei ya mafuta ya Taa ikisalia kama kawaida.

Oketch amesema hatua hiyo ni baada ya Hazina ya kitaifa kupunguza ushuru wa mafuta kwa asilimia 8 kutoka asilimia 13 ili kuchangia kupungua kwa gharama ya ununuzi wa mafuta baada serikali kutenga shilingi bilioni 6.5 za ruzuka ya mafuta.

Hatua hii imejiri mda mchache tu baada ya Mamlaka hiyo awali kutangaza bei ya mafuta ya Petroli kupanda kwa shilingi 28 kwa lita na mafuta ya Dizeli yakipanda kwa shilingi 40 kwa lita, hatua iliyosababisha viongozi wa upinzani kutishia kuitisha maandamano ya kitaifa kushinikiza kupunguzwa kwa bei hizo za mafuta nchini.

Hata hivyo katika taarifa ya Mamlaka ya EPRA, ilisema mafuta ya Petroli sasa yatauzwa kwa shilingi 197.60 kwa lita, huku mafuta ya Dizeli yakiungwa kwa shilingi 196.63 kwa lita na mafuta ya Taa yakisalia shilingi 152.78 kwa lita, katika jiji la Nairobi.

Mjini Mombasa, bei ya mafuta ya Petroli sasa itauzwa kwa shilingi 194.32, mafuta ya Dizeli yakiuzwa kwa shilingi 193.35 huku mafuta ya Taa yakiuzwa kwa shilingi 149.49 kwa lita na mjini Kilifi bei hiyo ya mafuta ikipungua na mafuta ya Petroli sasa yatauzwa kwa shilingi 195.18, mafuta ya Dizeli yakiuzwa kwa shilingi 194.22 huku mafuta ya Taa yakiuzwa kwa shilingi 150.36 kwa lita.

Hata hivyo Mamlaka hiyo imesema tangazo hilo limezingatia notisi ya kisheria nambari 70 na kwamba bei hiyo mpya ya mafuta inaanza kutekelezwa mara moja na itadumu kwa kipindi cha mwezi mmoja hadi tarehe 14 mwezi Mei mwaka huu.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Biashara ya Mananasi yakabiliwa na changamoto Kilifi

Published

on

By

Wafanyibiashara kuuza matunda aina ya Nanasi kaunti ya Kilifi wanasema biashara ya matunda hayo inazidi kudorora msimu huu ikilinganishwa na msimu uliopita.

Kulingana na wafanyibiashara hao, matunda ya Mananasi hayapatikana kwa urahisi sokoni kutokana na mabadiliko ya hali ya angani licha ya biashara ya matunda hayo kuwa na thamani kubwa katika soko la Pwani na taifa.

Wakiongozwa na Japhet Khambi, wafanyibiashara hao walisema kwa sasa wanategemea matunda hayo kutoka nje ya nchi hasa taifa la Uganda ambapo uagizaji wa matunda hayo umekuwa ghali mno.

Katika suala la usafirishaji wa bidhaa hiyo katika soko la kaunti ya Kilifi kutoka taifa hilo jirani la Afrika Mashariki, wafanyibiashara hao walisema ghamara ya usafiri uko juu mno hali ilichangia bei ya bidhaa hizo kuongezeka mara dufu.

“Hii mambo ya gharama ya usafirishaji na uhaba wa matunda hayo bei ya bidhaa hiyo imepanda kwa kiwango kikubwa, alieleza Khambi.

Wafanyibiashara wa matunda ya Mananasi walisema Nanasi ambalo lilikuwa Linanunuliwa kwa shilingi 100 sasa tunda hilo limepanda bei na kuuzwa kwa shilingi 250.

“ Tulikuwa tunanunua Mananasi kutoka eneo la Chakama katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi kwa bei nafuu lakini kwa sasa hayapatikani na kutulazimu kuangiza matunda kutoka Uganda.”, alisema Khambi.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

Bei za mafuta kuongezeka katikati ya mwezi aprili

Published

on

By

Kenya sasa inakabiliwa na hatari ya kupanda kwa bei za mafuta, huku mgogoro unaoendelea mashariki ya Kati ukianza kuathiri bei nchini.

Serikali sasa imeonya kuwa kufikia katikati ya mwezi Aprili, bei za mafuta huenda zikapanda ikionya kuwa ongezeko la bei ya mafuta kwa sasa haliwezi kuepukika kufuatia kupanda kwa bei za mafuta kimataifa.

Waziri wa hazina kuu ya kitaifa John Mbadi aliwahakikishia wakenya kuwa hakuna cha kuhofia kwani wameweka mikakati kupunguza athari zake.

Ili kupunguza athari za bei za mafuta kuongezeka, serikali ilisema itatumia shilingi bilioni 17 kutoka mfuko wa ada ya uwekezaji wa mafuta kusaidia kudhibiti bei kwa mda wa miezi 3 ijayo.

Kwa sasa serikali inasema kuna akiba ya kutosha ya mafuta na shehena zaidi zinatarajiwa nchini hivi karibuni.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending