Connect with us

Business

Wafanyabiashara wanataka wachuuzi kuondolewa Sokoni, Kilifi

Published

on

Wafanyabiashara wa soko la kwa Charo wa mae mjini kilifi kaunti ya Kilifi, wanaitaka serikali ya kaunti kuwaondoa wachuuzi wanaoendeleza biashara zao nje ya Soko hilo.

Wakiongozwa na Florence Kazungu, wafanyibiashara hao wanasema kuwa biashara imepungua kwani wateja wengi wananunua bidhaa nje ya soko hali inayofanya mapato yao kupungua.

Wamesema kuwa licha ya wao kulipa ushuru katika soko hilo, bidhaa zao zinasalia sokoni kutokana uhaba wa wateja hali inayowasababishia hasara kwani bidhaa nyingi huharibika.

Hata hivyo wanaitaka serikali ya kaunti kuingilia kati suala hili na kuwaondoa wachuuzi hao.

“Biashara iko chini wateja hawaingii sokoni kwa sababu wananunua bidhaa hapo nje ya soko hali inayotufanya tunasalia na bidhaa zetu hadi zinaharibika ili hali tunalipa ushuru, serikali inafaa iwatoe wachuuzi hao ili sisi nasi tuweze kupata riziki ya kila siku”. alisema Florence.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Mamlaka ya AFA yahimiza upanzi wa mkorosho

Published

on

By

Mamlaka ya Kilimo na Chakula nchini AFA, imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha taifa linaboresha mazao yake na kuchangia uzalishaji wa chakula nchini.

Hatua hii imechangia zaidi na mikakati endelevu ya kuwawezesha wakulima kufahamu mipango endelevu ya uimarishaji wa Kilimo cha sasa na kwa kuzingatia utumiaji wa mifumo bora ya kilimo.

Mamlaka hiyo ambapo inaendeleza kampeni ya kuhamisha wakulima kuhusu umuhimu wa kilimo cha Korosho imesisitiza haja ya ujumuishaji wa wakulima, wawekezaji na wadau mbalimbali ili kupiga jeki sekta ya Kilimo huku ikiahidi kuendeleza hamasa kwa jamii za kaunti za Pwani kuhusu kilimo cha korosho na utafutaji wa soko huru.

Katika Kongamano la kitaifa lililoandaliwa katika kaunti ya Kwale, Mamlaka hiyo iliwapa wakulima kutoka kaunti sita za Pwani miche ya mikorosho elfu mia moja katika juhudi za kukuza kilimo cha zao hilo nchini.

Katibu katika Idara ya Kilimo nchini Paul Kiprono, alisema mpango huo unalenga kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji wa korosho na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Kiprono alitoa wito kwa serikali za kaunti pamoja na wadau wa sekta ya kilimo kushirikiana kwa karibu ili kuboresha kilimo cha korosho.

“Kenya ilikuwa ikiongoza katika zao la mkorosho katika miaka ya 1990 lakini kutokana na changamoto za kibiashara zao hilo lilishuka katika masoko ya kimataifa kutokana na ukosefu wa kuwekezaji kwa wakulima lakini sasa tumeanza kupiga hatua kwani tunazalisha zaidi ya tan elfu 9 za korosho”, alisema Rono.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa AFA, Cornelly Serem, alisema mamlaka hiyo imejizatiti kuboresha kilimo cha korosho kupitia utoaji wa miche bora na mafunzo kwa wakulima ili kuongeza tija.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Business

Wafanyabiashara wa Korosho walalamikia kupanda kwa bei ya mafuta.

Published

on

By

Wafanyabiashara wa korosho katika soko la Oloetiptip mjini Kilifi kaunti ya Kilifi wanairai serikali kushughulikia suala la kupanda kwa bei ya mafuta.

Kulingana na wafanyibiashara hao wanasafirisha korosho kutoka kaunti ya Lamu hali na ni ghali sana.

Wakizungumza na mwanahabari wetu wafanyibiashara hao waliongeza kuwa gharama  ya usafirishaji imepanda kutokana na ongezeko la mafuta hali inayowapelekea kukadiria hasara.

Aidha wanasema bei ya korosho kwa  sasa imepanda kwa shilingi 130 ambapo pia wanasema itawalazimu kuongeza 200 ili wauze shilingi  1700 kwa kilo .

Wafanyibiashara hao  wamesema kuwa  imewalazimu kupandisha bei na hata kupunguza kiwango ili wapate faida ndogo kujikimu kimaisha.

Wameitaka serikali kuangazia upya swala la kupanda kwa gharama ya  mafuta ili kuwapunguzia hasara ambazo wanakadiria kwa sasa.

Wanasema eneo hili halina korosho kwa sasa zile zinaapatika ziko ghali huku wakiwataka wakulima kukumbatia kilimo cha kisasa ili kuongeza zao hilo.

“ Tunatoa korosho kutoka kaunti ya lamu na kutoka huko hadi huku nauli iko juu hali ambayo inatufanya tukiuza hatupati faida , na sai ambapo mafuta yamepanda bei nauli pia imepanda pia korosho zenyewe ziko ghali hali inayofanya biashara kuwa ngumu.

”Tunaiomba serikali inaangalie wafanyibiashara kwanu tunaumia sana.”

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Trending