Connect with us

News

Bodi ya Hazina ya fedha ya Mombasa yaapishwa

Published

on

Serikali ya kaunti ya Mombasa imeapisha rasmi bodi ya kwanza ya hazina ya fedha ya Mombasa, hatua inayoweka msingi wa utekelezaji wa sheria ya hazina hiyo ya mwaka wa 2026.

Hazina hiyo inalenga kutoa mikopo nafuu kwa wajasiriamali, vijana, wanawake, vyama vya ushirika, biashara ndogondogo kupitia mafunzo, uongozi bora na usimamizi wa fedha.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, gavana wa Mombasa Abdulswamad Sharif Nassir alisema bodi hiyo itaanza mara moja kuandaa mifumo ya utekelezaji ili kuhakikisha wafanyabiashara wanapata huduma za kifedha kwa wakati, hatua itakayochochea kuwepo na nafasi za ajira, kupanua fursa za kiuchumi na kuimarisha uchumi wa Mombasa.

Bodi hiyo itaongozwa na mwenyekiti Samuel Omondi Okech, huku Munira Hamisi akiwa Afisa Mkuu Mtendaji.

Bodi ya hazina ya fedha ya Mombasa kaunti ya Mombasa imeapishwa rasmi, chini ya uangalizi wa Gavana wa Mombasa Abdulswamad Sharrif Nassir

Wengine ni Elizabeth Sonia Michael, mwakilishi wa wanawake, Abduswamad Noor mwakilishi wa watu wenye uatilifu, Hamza Kombo mwakilishi wa vijana, Hamisi Kurichwa afisa Mkuu wa biashara na Swaleh Mwalizuma, afisa mkuu wa fedha na mipango ya uchumi.

Kuapishwa kwa bodi hiyo kunatajwa kuwa hatua muhimu katika juhudi za Serikali ya Kaunti ya Mombasa za kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika ukuaji wa uchumi na kunufaika na maendeleo ya kaunti.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

DCI wamtia nguvuni mshukiwa sugu Mombasa

Published

on

Maafisa wa upelelezi wa makosa ya jinai nchini (DCI) wamemtia mbaroni mshukiwa mmoja katika eneo la Kazandani, kaunti ya Mombasa kwa tuhuma za matumizi yasiyofaa ya mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na DCI, mshukiwa huyo Halima Ngache, maarufu kama Princess Halima, amekamatwa baada ya uchunguzi kubaini kuwa anahusishwa na akaunti ya mtandao wa X, (Twitter), ambayo inadaiwa kuchapisha taarifa nyeti kuhusu mienendo ya watu wanaolindwa na serikali.

DCI imesema kuwa suala hilo linachunguzwa kama tishio linalowezekana kwa usalama wa taifa.

Kwa sasa, mshukiwa anazuiliwa na anaendelea kufanyiwa taratibu za kisheria kabla ya kufikishwa mahakamani.

Wakati huo huo, DCI imewakumbusha wananchi kuwa ingawa Katiba inalinda uhuru wa kujieleza, haki hiyo inapaswa kutumiwa kwa uwajibikaji na kwa kuzingatia sheria ikiwahimiza wananchi kuepuka kusambaza taarifa zinazoweza kuhatarisha usalama wa watu wanaolindwa au kuchochea taharuki miongoni mwa umma.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
Continue Reading

News

Wanaume wahimizwa kuzungumzia matatizo yanayowakabili

Published

on

By

Mwezi wa Juni huwa umetengwa kimataifa kama mwezi wa kuhamasisha jamii kuhusu afya ya akili, huku kukiwa na msisitizo maalum wa Afya ya Akili kwa Wanaume (Men’s Mental Health Awareness Month).

Mwanzilishi wa shirika la MK initiative, Millicent Khayanga alisema wanaume wengi wanakabiliwa na hali ya msongo wa mawazo hali inayofanya baadhi yao kuchukua maamuzi mabaya kama ya kujitoa uhai.

Akizungumzia suala hilo baada ya kuongoza matembezi ya kutoa hamasa kuhusu afya ya akili kwa wanaume mjini Kilifi kaunti ya Kilifi, Millicent aliishinikiza jamii kutowachukulia kama watu wadhaifu wanapopaza sauti zao kutokana na changangomoto zinazowakabili.

“Jamii imefanya wanaume kutokuzungumzia changamoto zinazowakabili kutokana na dhana kuwa mwanamume hafai kuonyesha unyonge wake,” alisema Khayanga.

Kwa upande wa wadau wengine katika mchakato huu wa kutoa hamasa kwa wanaume kuhusu afya ya akili waliishinikiza serikali kutenga fedha maalumu za kuwawezesha wanaume kujikimu kimaisha ili kuwaepusha na hali hii.

Wanaharakati wa jamii wahimiza umuhimu wa mwezi wa kuhamasisha jamii kuhusu afya ya akili

Ni kauli ambazo ziliungwa mkono na Patrick Abio mkaazi wa Kilifi ambaye alisema ikiwa jamii itawakumbatia wanaume na kutowahukumu wanapozungumzia changamoto zinazowakabili itakuwa vyema kwani hatua hiyo itadhibiti visa vya msongo wa mawazo miongoni mwao pamoja na kuzuia visa vya kujitoa uhai.

“Ikiwa serikali, mashirika na jamii zitachukulia hili kwa uzito itakuwa afueni kubwa kwa wanaume ” Alisema Abio.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending