Connect with us

News

Tundu Lissu Atengwa na Wafungwa Wengine Gereza la Ukonga

Published

on

Kiongozi wa Chama Cha CHADEMA Tundu Lissu ametoa taarifa kuelezea hofu dhidi ya maisha yake,kufuatia hatua ya serikali na maafisa wa Gereza la Ukonga anakozuiliwa Lissu, ya kumhamishia chemba inayomtenga kabisa na wafungwa wengine wanakabiliwa na mashtaka ambayo adhabu yake ni Kifo.

Lissu anaitaja hatua hiyo kuwa ‘upweke wa kulazimishwa’

“Wafungwa wenzangu waliokuwa nami kwenye seli moja, ambao walikuwa wamehukumiwa adhabu ya kifo, wametolewa wote nimeachwa peke yangu,”Akasema Lissu.

Tundu Lissu akiwa kotini

Taarifa hiyo inaongeza kuwa seli hiyo imewekwa kamera za CCTV kurekodi kila kitu kinachoendelea selini humo, ikiwa ni pamoja na wakati anapobadilisha nguo au kujisaidia, hali inayomtia hofu zaidi kiongozi huyo wa CHADEMA.

“Sina faragha yoyote tena, na wala hili sio tena suala la usalama bali ni kudhalilishwa kwa utu wangu kama binadamu.” Akiongeza kusema Tundu Lissu.
Chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 12 na 13, zinazolinda hadhi ya mfungwa ni kinyume Cha Sheria na ukiukaji WA haki kupitia kuteswa au kudhalilishwa kwa mfungwa gerezani.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Aisha Jumwa akihama rasmi chama cha UDA

Published

on

By

Mgombea wa kiti cha ugavana wa kaunti ya Kilifi Aisha Jumwa amekihama rasmi chama cha UDA, akisema atatangaza baadaye mwelekeo atakaochukua wa kisiasa.

Jumwa alitoa tangazo hilo katika kikao na Wanahabari kilichofanyika katika makaazi yake, eneo la Kakuyuni huko Malindi kaunti ya Kilifi leo siku ya Alhamis.

Hatua ya Jumwa ilijiri baada ya kuwepo na tetesi kwamba alikuwa na mipango ya kuhama chama hicho kutokana na sintofahamu za kisiasa ndani ya chama cha UDA kuhusu msimamo wake wa kisiasa wa kuwania nafasi ya ugavana wa Kilifi.

Jumwa alilalamika kwamba alikuwa akinyanyaswa na baadhi ya viongozi hata kutimuliwa katika Ikulu ya rais licha ya kupambana katika kampeni za rais Ruto mwaka wa 2022, akionekana kumlaumu rais Ruto kwa kutomjali tena hata baada ya kusimama na yeye kisiasa.

Kiongozi huyo alikashfu vikali kutengwa katika mikutano ya UDA licha ya kuwa mwandani wa rais Ruto na pamoja na kufanyikisha miradi ya serikali mashinani, akisema tangu atangaze mchakato wa kuwania kiti cha ugavana wa Kilifi mwaka wa 2027, amekuwa akipitia masaibu mengi.

Hii sio mara ya kwanza kwa Jumwa kukihama Chama cha UDA na kurejea kwenye chama hicho, lakini hatua aliyoichukua sasa itabadili masimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi.

Itakumbukwa kwamba Jumwa amekuwa mwandani wa karibu wa rais William Ruto, lakini hatua aliyoichukua huenda ikabadili msimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi na Pwani kwa jumla. 

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Mahakama ya Kilifi yaagiza kuzuiliwa Washukiwa 7 wa mauaji

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imeagiza kuzuiliwa kwa siku 14 washukiwa 7 wanaotuhmiwa kuhusika katika kifo cha mwanamke mmoja aliyekuwa na umri wa miaka 65, ambaye aliuwawa kwa tuhma za uchawi katika eneo la Malomani eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi.

Washukiwa hao Gilbert Karisa Changawa, Selvestar Changawa Kahindi, Elizabeth Jackson Ngala, Dhahabu Kithi Kombe, Dzendere Palu Kalama, Agness Changawa na Kadzo Ngombo Bienge watazuiliwa katika kituo cha Bamba wakati uchunguzi ukiendelea.

Kulingana na Afisa mpelelezi kutoka kitengo cha DCI ameeleza mahakama kwamba ilikuwa mnamo tarehe 27 mwezi huu ambapo walipokea tarifa kwamba dama changawa alikuwa amekatwa kichwa na kuuwawa na watu wasiojulikana usiku huo.

Afisa mpelelezi pia ameeleza kuwa washukiwa ambao ni wanafamilia,siku kabla ya tukio husika walikuwa wameandaa kikao cha kudumisha Amani baada ya kifo kilichokuwa kimetokea kwa kijana mmoja mtoto wa mmoja kati ya washukiwa aliyefariki kaunti ya Mombasa baada ya kupigwa kwa tuhma za wizi.

Kutokana na kifo cha kijana huyo wanafamilia hao walimtuhmu dama kwamba ndiye aliyekuwa amemroga kijana huyo na kusababisha kifo hicho cha gafla, ambapo usiku huo Dama aliuwawa nyumbani kwake.

Washukiwa watarudishwa mahakamani tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu baada ya uchunguzi kukamilika.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Trending