News
Maelfu ya vijana wajitokeza kwa mradi wa NYOTA kaunti ya Kilifi
Maelfu ya vijana kutoka wadi mbalimbali eneo bunge la Kilifi kazkazini kaunti ya Kilifi wamehudhuria zoezi la kutibitisha majina ya wale waliofaulu katika mradi wa NYOTA.
Akizungumza na Wanahabari baada ya zoezi hilo, Katibu wa Wizara ya vijana nchini Fikirini Jacobs alisema mradi huo umelenga vijana 70 kwa kila wadi ambao watapokea shilingi elfu 50 kwa kila kijana ili kuanzisha biashara.
Jacobs aliongezea kwamba mradi huo utakaogharimu shilingi bilioni 20, unalenga vijana ambao walikosa nafasi za kuendeleza masomo yao baada ya kukamilisha kidato cha nne na darasa la 8 ambao bado wako chini ya umri wa miaka miaka 29.
“Huu mradi unalenga kuhakikisha vijana wa umri wa miaka 18 hadi 29 wananufaika na fedha hizi na zitapeanwa kuwa vijana na kila mmoja atapata shilingi elfu 50 za kuwasaidia,” alisema Fikirini.
Naye Naibu Kamishena wa eneo hilo Samuel Mutisya, aliwahimiza vijana kuchukua vitambulisho ili wasipitwe na nafasi za ajira zilizotangazwa na serikalini.
Kwa upande wao vijana waliohudhuria zoezi hilo wakiongozwa na Peter mweni, wameusifu mradi huo, wakisema utawasaidia kimaisha, japo wameitaka serikali kujumuisha vijana wote kwani kuwa wale waliosoma lakini hawana ajira.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

