Business
Wafanyabiashara wa Korosho walalamikia kupanda kwa bei ya mafuta.
Wafanyabiashara wa korosho katika soko la Oloetiptip mjini Kilifi kaunti ya Kilifi wanairai serikali kushughulikia suala la kupanda kwa bei ya mafuta.
Kulingana na wafanyibiashara hao wanasafirisha korosho kutoka kaunti ya Lamu hali na ni ghali sana.
Wakizungumza na mwanahabari wetu wafanyibiashara hao waliongeza kuwa gharama ya usafirishaji imepanda kutokana na ongezeko la mafuta hali inayowapelekea kukadiria hasara.
Aidha wanasema bei ya korosho kwa sasa imepanda kwa shilingi 130 ambapo pia wanasema itawalazimu kuongeza 200 ili wauze shilingi 1700 kwa kilo .
Wafanyibiashara hao wamesema kuwa imewalazimu kupandisha bei na hata kupunguza kiwango ili wapate faida ndogo kujikimu kimaisha.
Wameitaka serikali kuangazia upya swala la kupanda kwa gharama ya mafuta ili kuwapunguzia hasara ambazo wanakadiria kwa sasa.
Wanasema eneo hili halina korosho kwa sasa zile zinaapatika ziko ghali huku wakiwataka wakulima kukumbatia kilimo cha kisasa ili kuongeza zao hilo.
“ Tunatoa korosho kutoka kaunti ya lamu na kutoka huko hadi huku nauli iko juu hali ambayo inatufanya tukiuza hatupati faida , na sai ambapo mafuta yamepanda bei nauli pia imepanda pia korosho zenyewe ziko ghali hali inayofanya biashara kuwa ngumu.
”Tunaiomba serikali inaangalie wafanyibiashara kwanu tunaumia sana.”
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Wafanyibiashara wa mitumba eneo la Diani wafunga biashara zao
Wafanyibiashara wa mitumba katika soko la Diani, kaunti ya Kwale, wamelazimika kufunga biashara zao kutokana na kudorora kwa shughuli za kibiashara katika kipindi hiki cha msimu wa watalii wachache na mvua zinazoendelea kushuhudiwa katika eneo hilo.
Wafanyabiashara hao wanasema idadi ya wanunuzi imepungua kwa kiasi kikubwa, hali iliyosababisha nguo nyingi kukosa soko.
Kulingana na wafanyibiashara hao wanategemea zaidi watalii wa ndani na nje na kutokana na msimu huu kuwa uko uko chini wateja wamepungua hali inayofanya maisha kuwa mgumu.
Wanasema wamelazimika kutupa baadhi ya nguo kwani zimesalia sokoni kwa muda mrefu hadi zingingine kuharibika, jambo ambalo limepelekea kupata hasara kubwa.
Aidha, wameongeza kuwa bei ya nguo za mitumba imeendelea kupanda ambapo wananunua ngunia moja kwa shilingi elfu 40 huku mauzo yakizidi kushuka.
“ Biashara imedorora sai kwani hakuna wateja ikizingatiwa kuwa tunategemea sana watalii na sasa hakuna wageni hata imetulazimu kutupa nguo kwani ngigi zimeharibika baada ya kukaa kwa mda mrefu bila kununuliwa”.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Mamlaka ya AFA yahimiza upanzi wa mkorosho
Mamlaka ya Kilimo na Chakula nchini AFA, imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha taifa linaboresha mazao yake na kuchangia uzalishaji wa chakula nchini.
Hatua hii imechangia zaidi na mikakati endelevu ya kuwawezesha wakulima kufahamu mipango endelevu ya uimarishaji wa Kilimo cha sasa na kwa kuzingatia utumiaji wa mifumo bora ya kilimo.
Mamlaka hiyo ambapo inaendeleza kampeni ya kuhamisha wakulima kuhusu umuhimu wa kilimo cha Korosho imesisitiza haja ya ujumuishaji wa wakulima, wawekezaji na wadau mbalimbali ili kupiga jeki sekta ya Kilimo huku ikiahidi kuendeleza hamasa kwa jamii za kaunti za Pwani kuhusu kilimo cha korosho na utafutaji wa soko huru.
Katika Kongamano la kitaifa lililoandaliwa katika kaunti ya Kwale, Mamlaka hiyo iliwapa wakulima kutoka kaunti sita za Pwani miche ya mikorosho elfu mia moja katika juhudi za kukuza kilimo cha zao hilo nchini.
Katibu katika Idara ya Kilimo nchini Paul Kiprono, alisema mpango huo unalenga kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji wa korosho na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Kiprono alitoa wito kwa serikali za kaunti pamoja na wadau wa sekta ya kilimo kushirikiana kwa karibu ili kuboresha kilimo cha korosho.
“Kenya ilikuwa ikiongoza katika zao la mkorosho katika miaka ya 1990 lakini kutokana na changamoto za kibiashara zao hilo lilishuka katika masoko ya kimataifa kutokana na ukosefu wa kuwekezaji kwa wakulima lakini sasa tumeanza kupiga hatua kwani tunazalisha zaidi ya tan elfu 9 za korosho”, alisema Rono.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa AFA, Cornelly Serem, alisema mamlaka hiyo imejizatiti kuboresha kilimo cha korosho kupitia utoaji wa miche bora na mafunzo kwa wakulima ili kuongeza tija.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

