Connect with us

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Bodi ya Hazina ya fedha ya Mombasa yaapishwa

Published

on

Serikali ya kaunti ya Mombasa imeapisha rasmi bodi ya kwanza ya hazina ya fedha ya Mombasa, hatua inayoweka msingi wa utekelezaji wa sheria ya hazina hiyo ya mwaka wa 2026.

Hazina hiyo inalenga kutoa mikopo nafuu kwa wajasiriamali, vijana, wanawake, vyama vya ushirika, biashara ndogondogo kupitia mafunzo, uongozi bora na usimamizi wa fedha.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, gavana wa Mombasa Abdulswamad Sharif Nassir alisema bodi hiyo itaanza mara moja kuandaa mifumo ya utekelezaji ili kuhakikisha wafanyabiashara wanapata huduma za kifedha kwa wakati, hatua itakayochochea kuwepo na nafasi za ajira, kupanua fursa za kiuchumi na kuimarisha uchumi wa Mombasa.

Bodi hiyo itaongozwa na mwenyekiti Samuel Omondi Okech, huku Munira Hamisi akiwa Afisa Mkuu Mtendaji.

Bodi ya hazina ya fedha ya Mombasa kaunti ya Mombasa imeapishwa rasmi, chini ya uangalizi wa Gavana wa Mombasa Abdulswamad Sharrif Nassir

Wengine ni Elizabeth Sonia Michael, mwakilishi wa wanawake, Abduswamad Noor mwakilishi wa watu wenye uatilifu, Hamza Kombo mwakilishi wa vijana, Hamisi Kurichwa afisa Mkuu wa biashara na Swaleh Mwalizuma, afisa mkuu wa fedha na mipango ya uchumi.

Kuapishwa kwa bodi hiyo kunatajwa kuwa hatua muhimu katika juhudi za Serikali ya Kaunti ya Mombasa za kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika ukuaji wa uchumi na kunufaika na maendeleo ya kaunti.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

DCI wamtia nguvuni mshukiwa sugu Mombasa

Published

on

Maafisa wa upelelezi wa makosa ya jinai nchini (DCI) wamemtia mbaroni mshukiwa mmoja katika eneo la Kazandani, kaunti ya Mombasa kwa tuhuma za matumizi yasiyofaa ya mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na DCI, mshukiwa huyo Halima Ngache, maarufu kama Princess Halima, amekamatwa baada ya uchunguzi kubaini kuwa anahusishwa na akaunti ya mtandao wa X, (Twitter), ambayo inadaiwa kuchapisha taarifa nyeti kuhusu mienendo ya watu wanaolindwa na serikali.

DCI imesema kuwa suala hilo linachunguzwa kama tishio linalowezekana kwa usalama wa taifa.

Kwa sasa, mshukiwa anazuiliwa na anaendelea kufanyiwa taratibu za kisheria kabla ya kufikishwa mahakamani.

Wakati huo huo, DCI imewakumbusha wananchi kuwa ingawa Katiba inalinda uhuru wa kujieleza, haki hiyo inapaswa kutumiwa kwa uwajibikaji na kwa kuzingatia sheria ikiwahimiza wananchi kuepuka kusambaza taarifa zinazoweza kuhatarisha usalama wa watu wanaolindwa au kuchochea taharuki miongoni mwa umma.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
Continue Reading

Trending