News
Aisha Jumwa akihama rasmi chama cha UDA
Mgombea wa kiti cha ugavana wa kaunti ya Kilifi Aisha Jumwa amekihama rasmi chama cha UDA, akisema atatangaza baadaye mwelekeo atakaochukua wa kisiasa.
Jumwa alitoa tangazo hilo katika kikao na Wanahabari kilichofanyika katika makaazi yake, eneo la Kakuyuni huko Malindi kaunti ya Kilifi leo siku ya Alhamis.
Hatua ya Jumwa ilijiri baada ya kuwepo na tetesi kwamba alikuwa na mipango ya kuhama chama hicho kutokana na sintofahamu za kisiasa ndani ya chama cha UDA kuhusu msimamo wake wa kisiasa wa kuwania nafasi ya ugavana wa Kilifi.
Jumwa alilalamika kwamba alikuwa akinyanyaswa na baadhi ya viongozi hata kutimuliwa katika Ikulu ya rais licha ya kupambana katika kampeni za rais Ruto mwaka wa 2022, akionekana kumlaumu rais Ruto kwa kutomjali tena hata baada ya kusimama na yeye kisiasa.
Kiongozi huyo alikashfu vikali kutengwa katika mikutano ya UDA licha ya kuwa mwandani wa rais Ruto na pamoja na kufanyikisha miradi ya serikali mashinani, akisema tangu atangaze mchakato wa kuwania kiti cha ugavana wa Kilifi mwaka wa 2027, amekuwa akipitia masaibu mengi.
Hii sio mara ya kwanza kwa Jumwa kukihama Chama cha UDA na kurejea kwenye chama hicho, lakini hatua aliyoichukua sasa itabadili masimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi.
Itakumbukwa kwamba Jumwa amekuwa mwandani wa karibu wa rais William Ruto, lakini hatua aliyoichukua huenda ikabadili msimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi na Pwani kwa jumla.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Mahakama ya Kilifi yaagiza kuzuiliwa Washukiwa 7 wa mauaji
Mahakama ya Kilifi imeagiza kuzuiliwa kwa siku 14 washukiwa 7 wanaotuhmiwa kuhusika katika kifo cha mwanamke mmoja aliyekuwa na umri wa miaka 65, ambaye aliuwawa kwa tuhma za uchawi katika eneo la Malomani eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi.
Washukiwa hao Gilbert Karisa Changawa, Selvestar Changawa Kahindi, Elizabeth Jackson Ngala, Dhahabu Kithi Kombe, Dzendere Palu Kalama, Agness Changawa na Kadzo Ngombo Bienge watazuiliwa katika kituo cha Bamba wakati uchunguzi ukiendelea.
Kulingana na Afisa mpelelezi kutoka kitengo cha DCI ameeleza mahakama kwamba ilikuwa mnamo tarehe 27 mwezi huu ambapo walipokea tarifa kwamba dama changawa alikuwa amekatwa kichwa na kuuwawa na watu wasiojulikana usiku huo.
Afisa mpelelezi pia ameeleza kuwa washukiwa ambao ni wanafamilia,siku kabla ya tukio husika walikuwa wameandaa kikao cha kudumisha Amani baada ya kifo kilichokuwa kimetokea kwa kijana mmoja mtoto wa mmoja kati ya washukiwa aliyefariki kaunti ya Mombasa baada ya kupigwa kwa tuhma za wizi.
Kutokana na kifo cha kijana huyo wanafamilia hao walimtuhmu dama kwamba ndiye aliyekuwa amemroga kijana huyo na kusababisha kifo hicho cha gafla, ambapo usiku huo Dama aliuwawa nyumbani kwake.
Washukiwa watarudishwa mahakamani tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu baada ya uchunguzi kukamilika.
Taarifa ya Teclar Yeri
News
Joho asitisha shughuli za uchimbaji madini za kampuni ya Tata Chemials Magadi
Serikali imesitisha shughuli zote za uchimbaji madini kwa kampuni ya Tata Chemials Magadi limited kwa kukiuka sheria za uchimbaji madini.
Kwenye taarifa iliyotolewa na Waziri wa madini na uchumi wa raslimali za baharini na maziwa Ali Hassan Joho ilisema kuwa hatua hiyo inafuatia majadiliano ya miaka mingi kati ya idara ya uchimbaji madini na kampuni hiyo kuhusu wajibu wake katika kutekeleza sheria ya uchimbaji madini.
Joho alisema bado kuna masuala muhimu ya kuzingatia sheria ambayo hayajatimizwa, ikiwemo kutokuwa na mkakati wazi wa kuongeza thamani ya madini, kutolipwa kwa malipo ya mrabaha na upatanishi, ripoti zisizokamili za mauzo ya nje, utekelezaji duni wa mikataba ya maendeleo ya Jamii, ukosefu wa ajira na mianya iliyoko katika utunzaji wa mazingira.
Waziri Joho, aliamuru kampuni hiyo kuwasilisha ushahidi wa kuzingatia sheria zote kikamilifu na kulipa madeni yoyote yaliyosalia kabla ya shughuli za uchimbaji madini kuanza tena.
Taarifa ya Janet Mumbi

