Connect with us

News

Paul Biya mwenye umri wa miaka 92 ameshinda uchaguzi wa urais Cameroon

Published

on

Tume ya uchaguzi nchini Cameroon imemtangaza Rais Paul Biya mwenye umri wa miaka 92 kama mshindi wa uchaguzi mkuu wa urais uliyofanyika Oktaba 12 mwaka huu.

Biya alishindi uchaguzi huo kwa kupata asilimia 53.7 ya kura zilizopigwa huku mpinzani wake wa karibu Issah Tchiroma akipata asilimia 35.2.

Biya anachukua hatamu ya uongozi kwa muhula wa wanane ambayo inajumuisha miaka 43 ya utawala, tangu alipoingia madarakani mwaka 1982.

Kutangazwa Rais Paul Biya kuwa mshindi wa uchaguzi huo kulisababisha vurugu, ghasia na machafuko nchini humo na kusababisha watu wanne kupoteza maisha yao baada yaku pigwa risasi na maafisa wa kukabiliana na ghasia.

Mchafuko hayo yametokana na shinikizo kutoka kwa raia wanamtaka Biya ajiuzulu kama rais wa taifa hilo la Afrika magharibi, kwani shinikizo kama hizo zimetolewa na mpinzani wake wa karibu wa kisiasa Issa Tchiroma ambaye alidai kwamba uchaguzi huo ulikumbwa na wizi wa kura.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending