Connect with us

News

Mpango wa uagizaji mafuta wa G to G waingia dosari

Published

on

Serikali imeendelea kujitetea kuhusu mpango wa uagizaji wa mafuta wa serikali kwa serikali maarufu kama G to G, huku viongozi wa kisiasa wakitoa mitazamo kinzani kuhusu utekelezaji wake.

Serikali kupitia Mamlaka ya kudhibiti bei za mafuta nchini EPPRA, imetangaza ongezeko la bei mpya za mafuta kwa shilingi 28 kwa lita moja ya mafuta ya petrol huku diseli ikiongezeka kwa shilingi 40 kwa lita.

Hatua hii imezua mjadala mkali kuhusu athari za mfumuko wa bei nchini.

Viongozi wa upinzani wakiongozwa na Kinara wa Chama cha DCP, Rigathi Gachagua, na Kinara wa Chama cha Wiper Kalonzo Musyoka wamekosoa vikali serikali kufutia ongezeko la bei ya mafuta wakisema mpango wa G to G ilikuwa ni njama ya kumfaidi Rais William Ruto, wakifichua kwamba takriban shilingi tano kwa kila lita ya mafuta itakayouzwa nchini itakuwa inamfaidi Rais Ruto.

Viongozi hao pia, walimtaka Waziri wa Kawi na Petroli nchini Opiyo Wandayi, pamoja na Waziri wa Biashara na Uwekezaji wa viwanda nchini Lee Kinyanjui, kujiuzulu.

Kwa upande wake mbunge wa Kiharu, Ndindi Nyoro pia ameukosoa mpango huo akidai kwamba ni njama ya baadhi ya viongozi wakuu serikalini kujinufaisha binafsi.

Nyoro aliema mpango huo ni njia ya kuwahadaa wakenya ilhali mzigo mkubwa unaishia kwa walipa ushuru.

Aliongeza kuwa mpango huo unanufaisha baadhi ya kampuni za mafuta nchini zinazodaiwa kumilikiwa na viongozi wa juu serikalini huku akitoa baadhi ya mapendekezo kwa serikali pamoja na wadau wa sekta ya kawi ambayo kulingana naye, yanaweza kushusha bei ya mafuta kwa takriban shilingi 27.

Hata hivyo, Rais William Ruto ametetea mpango huo akisema serikali imetumia takriban shilingi bilioni 6.5 kutoa ruzuku ya mafuta ili kupunguza mzigo kwa wananchi hasa ushuru wa VAT kwa asilimia 8.

Kwa upande wake, Waziri wa Kawi na Petroli nchini Opiyo Wandayi alisema serikali imejizatiti kukabiliana na wanaojihusisha na uagizaji wa mafuta ghushi humu nchini.

Hata hivyo, kumeshuhudiwa tofauti katika takwimu za fedha zilizotolewa kuhusu mpango huo, Rais akitaja bilioni 6.5 ilhali Waziri Wandayi akisema serikali iliwekeza takriban bilioni 6.2.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending