News
Kaunti ya Kilifi yajitenga na shutma za Aisha Jumwa
Serikali ya kaunti ya Kilifi imejitenga na vurugu zilizoshuhudiwa wakati wa mazishi ya Afisa wa kaunti katika eneo la Msabaha wadi ya Ganda eneo bunge la Malindi siku ya Jumatatu.
Akizungumza na vyombo vya habari, Naibu gavana wa Kilifi Flora Mbetsa Chibule, alidai kwamba wanasiasa wenye malengo fiche walitumia hafla ya mazishi na kutangaza semi za uongo kuhusu msaada wa kaunti kwa familia ya mwendazake.
Chibule alitangulia kwa kuomba msamaha kwa familia ya marehemu na kukariri kuwa serikali ya kaunti kupitia gavana Gedion Mung’aro awali iliwasiliana na familia kuhusu namna ya kuipa msaada, japo haukuwekwa hadharani.
Wakati huo huo Chibule alidokeza kwamba gavana Mung’aro binasfi alitoa msaada wake wa fedha kwa familia ya marehemu.
“Huyu ni mfanyakazi wa serikali ya kaunti mbali na mstahiki gavana wetu, idara ya ugatuzi na utekelezaji ilichangia kwa mambo hayo ya mazishi, alipokuwa na anaenda kuangaliwa maisha yake kule Moshi mustahiki gavana mwenyewe alitoa nusu milioni kumsaidi Baloteli(marehemu), nilikwenda pale tukaramuka(kuomboleza) tukasema mama madamu unahii shahada tutakutafutia nafasi katika serikali ya kaunti”, alisema Chibule.
Vile vile naibu gavana huyo aliwapa changamoto viongozi wa siasa kuheshimu hafla za mazishi na kupunguza siasa hasa wanapoalikwa katika hafla hizo.
“Jana Msabaha mfanyakazi wetu shupavu almaarufu Baloteli nikwamasikitiko makuu ya kwamba matokeo ya mazishi yale yalikwenda vile yalivyo sisi kama serikali ya kaunti tunaomba msamaha kwa familia, kwa mama Mbeyu tusamehe kwa jinsi shughuli ilivyokuwa, viongozi wenzangu tafadhali mazishi yaheshimiwe”, alisistiza naibu gavana Chibule.
Katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa bodi ya kitaifa ya barabara Aisha Jumwa alitoa changamoto kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kumpa ajira mke wa Marehemu kauli ambayo iliibua hisia miongoni mwa viongozi na kusababisha rabsha.
“Nimesikiza viongozi wa kaunti hapa mmoja mpaka wa mwisho wakizungumza, sikupata hata mmoja mwenye huruma aseme Baloteli ametumikia kaunti na hivi amefariki mkewe Maurine jumatatu au jumanne ako kazini, sikusikia, lakini mimi nilikuwa nimevipanga, mmkuja matangani na kama mmempangia simzunguze kila mtu asikie, lakini kwa sababu havikuzungumiziwa nimevipatia wiki moja kama hatapata kazi nitarejea hapa maana mwanijua mimi ni mtu wa matendo”, alisema Jumwa.
Taarifa ya Joseph Jira