Sports
Kilabu MTG United Imezindua Wachezaji 8 Wapya kabila ya msimu wa NSL
Kilabu ya MTG United ya akina dada ya kaunti ya Kilifi inayoshiriki Ligi ya daraja la Pili NSL imewatambulisha wachezaji wanane wapya kuelekea msimu mpya. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo kinara ambaye pia ni naibu Gavana wa Kaunti ya Kilifi Flora Mbetsa Chibule amehakikishia Timu hiyo kwamba atatembea nao katika mechi Zote za Ligi msimu wa mwaka 2025/26.
“Nitahahakisha ninatembea nanyi katika kila mechi msimu huu,kuanzia na ya kwanza kule Kwale Oktoba 5 ,mimi na wenzangu tutakuja kuwasapoti kilabu yetu kufanya vizuri,kila ushindi mtakayopata nitaongeza posho.”
Mkurugenzi mkuu katika wizara ya michezo Boniface Kirimi amesema kwamba wizara pamoja na kaunti ziko tayari kuinua vipaji akisema kwamba serikali hiyo imo mbioni kuboresha miondo msingi.
“Kwa sasa serikali ya kaunti iko katika hatua ya mwisho mwisho kuendeleza ujenzi wa Uga wa Waters ,tunaunda pia viwanja viwili vya mchezo wa mpira wa vikapu na juzi tumekutana na shirikisho la FKF Kaunti ya Kilifi kuiweka mikakati ya kuboresha miondo misingi ya soka na kuwashika mkono vilabu vyetu.”