Connect with us

Sports

Kilabu MTG United Imezindua Wachezaji 8 Wapya kabila ya msimu wa NSL

Published

on

Kilabu ya MTG United ya akina dada ya kaunti ya Kilifi inayoshiriki Ligi ya daraja la Pili NSL imewatambulisha wachezaji wanane wapya kuelekea msimu mpya. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo kinara ambaye pia ni naibu Gavana wa Kaunti ya Kilifi Flora Mbetsa Chibule amehakikishia Timu hiyo kwamba atatembea nao katika mechi Zote za Ligi msimu wa mwaka 2025/26.

“Nitahahakisha ninatembea nanyi katika kila mechi msimu huu,kuanzia na ya kwanza kule Kwale Oktoba 5 ,mimi na wenzangu tutakuja kuwasapoti kilabu yetu kufanya vizuri,kila ushindi mtakayopata nitaongeza posho.”

Mkurugenzi mkuu katika wizara ya michezo Boniface Kirimi amesema kwamba wizara pamoja na kaunti ziko tayari kuinua vipaji akisema kwamba serikali hiyo imo mbioni kuboresha miondo msingi.

“Kwa sasa serikali ya kaunti iko katika hatua ya mwisho mwisho kuendeleza ujenzi wa Uga wa Waters ,tunaunda pia viwanja viwili vya mchezo wa mpira wa vikapu na juzi tumekutana na shirikisho la FKF Kaunti ya Kilifi kuiweka mikakati ya kuboresha miondo misingi ya soka na kuwashika mkono vilabu vyetu.”

Afisa mkuu mtendaji wa MTG United Dorcas Amakobe amesema kwamba msimu huu wameweka mikakati kuhakikisha kwamba kilabu hiyo inapata ufanisi uwanjani akiahidi kwamba akina dada hao kando na kulipwa mshahara watapata marupurupu katika kila mechi wanayoshiriki.
“Ili timu yetu iweze kushiriki kikamilifu na kupata matokeo chanya kama shirika tumeamua kutenga kilabu ya MTG kupata maslahi ya kipekee kama idara,natoa ahadi pia kwamba kando na mishahara hawa wanadada watapata marupurupu ili kuwapa hamasa katika mechi zao.”
Kwa upande wake Kocha wa MTG United Fatima Khamis marufu coach Tibu ameahidi kupaisha Kilabu hiyo Hadi kileleni wakisaka tiketi ya ligi kuu Akina dada FKF WPL.
“Nina matumaini msimu ujao tunamaliza ya kwanza ama ya pili,lakini pia nimshukuru naibu gavana Chibule kwa kusapoti timu kwa hali na mali msimu jana,tumeweza kusajili wachezaji wanane wapya kwa ajili ya msimu mpya na tuna matumaini watatupa matokeo chanya.”
MTG United walimaliza nafasi ya Saba msimu wa mwaka 2025/26
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending