Sports
Kilabu MTG United Imezindua Wachezaji 8 Wapya kabila ya msimu wa NSL
Kilabu ya MTG United ya akina dada ya kaunti ya Kilifi inayoshiriki Ligi ya daraja la Pili NSL imewatambulisha wachezaji wanane wapya kuelekea msimu mpya. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo kinara ambaye pia ni naibu Gavana wa Kaunti ya Kilifi Flora Mbetsa Chibule amehakikishia Timu hiyo kwamba atatembea nao katika mechi Zote za Ligi msimu wa mwaka 2025/26.
“Nitahahakisha ninatembea nanyi katika kila mechi msimu huu,kuanzia na ya kwanza kule Kwale Oktoba 5 ,mimi na wenzangu tutakuja kuwasapoti kilabu yetu kufanya vizuri,kila ushindi mtakayopata nitaongeza posho.”
Mkurugenzi mkuu katika wizara ya michezo Boniface Kirimi amesema kwamba wizara pamoja na kaunti ziko tayari kuinua vipaji akisema kwamba serikali hiyo imo mbioni kuboresha miondo msingi.
“Kwa sasa serikali ya kaunti iko katika hatua ya mwisho mwisho kuendeleza ujenzi wa Uga wa Waters ,tunaunda pia viwanja viwili vya mchezo wa mpira wa vikapu na juzi tumekutana na shirikisho la FKF Kaunti ya Kilifi kuiweka mikakati ya kuboresha miondo misingi ya soka na kuwashika mkono vilabu vyetu.”
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

