Connect with us

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Bingwa wa Afrika mbio za mita 100 mkenya Ferdinand Omanyala azidi kuthibitisha ubora wake mbio Botswana Golden Grand Prix akimaliza wa pili na sekunde 9.95

Published

on

By

Mwanariadha mwenye kasi zaidi barani Afrika, Ferdinand Omanyala, amethibitisha kurejea kwake katika kiwango cha juu kwa mbio za kuvutia za sekunde 9.95 kwenye mashindano ya Botswana Golden Grand Prix yaliyofanyika Jumapili, Aprili 26 jijini Gaborone.

Katika fainali ya wanaume ya mita 100 iliyokuwa na ushindani mkali, Mkanada Jerome Blake alishinda kwa sekunde 9.93, huku mwenzake Andre De Grasse na Omanyala wakitumia sekunde 9.95 katika ushindani wa karibu sana. Ingawa awali ilionekana kama nafasi ya pili iligawanywa, matokeo rasmi yalimweka Omanyala katika nafasi ya tatu kwa tofauti ndogo sana.

Licha ya nafasi hiyo, matokeo hayo yaliashiria mbio ya tatu mfululizo kwa Omanyala kukimbia chini ya sekunde 10 ndani ya siku saba tu, na kukamilisha kurejea kwa nguvu kwa mshikiliaji wa rekodi ya Afrika. Mkenya huyo alianza mfululizo huo kwa ushindi wa sekunde 9.98 katika Addis Ababa Grand Prix Aprili 18, kabla ya kuwapa mashabiki wa nyumbani burudani kwa ushindi wa sekunde 9.96 katika mashindano ya Kip Keino Classic jijini Nairobi Aprili 24.

Mfululizo huu wa matokeo unaashiria kurejea kwa nguvu kwa Omanyala baada ya msimu mgumu wa 2025 uliokumbwa na majeraha na kutokuwepo kwa uthabiti, ambapo alishindwa kushuka chini ya kiwango muhimu cha sekunde 10.

Sasa macho yanaelekezwa kwenye World Athletics Relays zitakazofanyika Mei 2–3, pia jijini Gaborone, ambapo Omanyala anatarajiwa kuiongoza timu ya Kenya katika mbio za kupokezana vijiti za 4x100m. Mashindano hayo yatakuwa hatua muhimu kuelekea kufuzu kwa michuano ya Ultimate Championship itakayofunga msimu.

Kwa kuzingatia mashindano yajayo ya Continental Tour Gold na michuano mikubwa kama Michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Glasgow, kurejea huku kwa kasi kwa Omanyala kumekuja wakati muafaka anapojenga upya kasi yake dhidi ya wanariadha bora duniani.

Continue Reading

Sports

Mkufunzi wa Klabu ya mancity Pep Guardiola amesifia jinsi ambayo timu yake ilifuzu fainali ya nne mfululizo kombe la FA

Published

on

By

Mkufunzi wa klabu ya Mancity Pep Guardiola ameisifia mafanikio yao ya kuwa timu ya kwanza kufika fainali nne mfululizo za FA Cup baada ya kurejea kwa nguvu mwishoni na kuinyima Southampton ushindi wa kushtukiza katika uwanja wa Wembley.

Klabu ya Southampton walikuwa wakielekea kufuzu kwa fainali yao ya kwanza baada ya miaka 23 wakati Finn Azaz alipofunga bao zuri na kuipa timu hiyo ya Championship uongozi dakika 11 kabla ya muda kuisha.

Hata hivyo, City walisawazisha haraka kupitia kwa Jeremy Doku kabla ya Nico Gonzalez kufunga bao la kuvutia na kuwapa ushindi wa 2-1 katika nusu fainali hiyo.

Kikosi cha Guardiola kimepoteza fainali mbili zilizopita za FA Cup dhidi ya Crystal Palace na Manchester United, huku wakiwashinda Manchester United mwaka 2023.

City, ambao watakutana na Chelsea katika fainali, sasa wako kwenye nafasi nzuri ya kushinda mataji matatu ya ndani.

Wachezaji wa Guardiola walitwaa Kombe la Ligi mwezi uliopita na kwa sasa wako kwenye ushindani mkali wa ubingwa wa Ligi Kuu dhidi ya Arsenal.

“Hakuna timu iliyofika fainali nne mfululizo. Ni jambo la ajabu na tunatumaini tutafika tukiwa na kasi nzuri,” alisema Guardiola.

Uamuzi wa kocha wa City kufanya mabadiliko nane kutoka kikosi kilichoishinda Burnley 1-0 Jumatano ulionekana kuwa wa kutiliwa shaka, huku Southampton wakitawala kipindi cha kwanza.

Hata hivyo, kikosi cha Guardiola kiliboresha mchezo wao sana baada ya mapumziko na kusaidiwa na kuingia kwa Doku, Erling Haaland na Bernardo Silva kutoka benchi.

“Ilikuwa ngumu lakini winga (Doku na Savinho) walipoingia walibadilisha kasi ya mchezo,” aliongeza Guardiola.

“Mara ya kwanza walipovuka mstari wa katikati walitengeneza bao la kushangaza. Soka huwa halitabiriki lakini namna tulivyocheza kipindi cha pili ilikuwa ya kipekee.”

Continue Reading

Trending