Connect with us

News

Zawadi: Ni wakati ubunge wa Ganze kuongozwa na Mwanamke

Published

on

Mwanasiasa Zawadi Kingi amekosoa uongozi duni unaondelea kushuhudiwa katika eneo bunge la Ganze, akisema viongozi walio mamlakani wameonyesha wazi kushindwa kutimiza malengo ya wananchi.

Akizungumza katika eneo bunge la Ganze, Zawadi amesema wakati umefika sasa kwa wakaazi wa Ganze kufungua macho na kutathmini uongozi wa mwanamke, akisema viongozi waliokuwa wakichaguliwa wameshindwa kufanikisha maendeleo mashinani.

Zawadi ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha ubunge wa Ganze wakati wa uchaguzi mkuu ujao mwaka wa 2027, ameahidi kulitatua suala la elimu, afya, sawa na kuendeleza miradi mingine muhimu, akisisitiza kwamba eneo bunge la Ganze linahitaji kiongozi Mwanamke.

“Wamekuwa kwa uongozi lakini hakuna walichofanyia wananchi wa Ganze, Ndovu wamekuwa wakiharibu mimea ya watu na hakuna suluhu lililotolewa, hospitali hazina madawa, maji ni changamoto na tena tuko na viongozi. Nawaomba munichague ili tubadilishe uongozi huu mabaya, wakati huo mwanamke anaweza”, alisema Zawadi

Zawadi alisema wakaazi wa Ganze wana jukumu la kutafakari na mapema kuhusu hatma yao ya maendeleo na kufanya maamuzi bora wakati wa uchaguzi, akiwarai wakaazi wa Ganze kutokubali kushawishiwa kisiasa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

NCTC yaanzisha hamasa mashinani kudhibiti ugaidi

Published

on

By

Kituo cha kitaifa cha kukabiliana na ugaidi yaani National Counter Terrorism Centre (NCTC) kimeanzisha mpango wa kutoa hamasa za kuwaepusha wananchi na masuala ya ugaidi hasa maeneo ya Shakahola katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Akizungumza katika eneo hilo, Afisa mkuu wa kituo hicho Grace Kaparo aliwataka wazazi kufuatilia kwa ukaribu mienendo ya watoto wao kama njia mojawapo ya kuzuia michipuko ya makundi ya ugaidi.

Kaparo alidokeza kwamba mpango huo unalenga kupunguza visa vya uhalifu miongoni mwa vijana sambamba na kuwajengea mustakabali bora wa maisha yao.

Hamasa hiyo inajiri baada ya kushughudiwa maafa ya watu zaidi ya 400 katika msitu wa Shakahola kutokana na mafunzo ya itikadi kali huku mshukiwa mkuu wa mauaji hayo akiwa katika mikono ya maafisa wa polisi.

“Tumekuja Shakahola kuelimisha jamii kuepusha makundi ya kigaidi na jinsi ya kutambua watu walio na itikadi kali ili kuepusha watu kuangamia kama hapa Shakahola watu wangekuwa na ufahamu wangeepuka maafa”, alisema Grace.

Kwa upande wake Naibu Kamishna eneo Malindi kaunti ya Kilifi Harrison Matevwa aliwataka maafisa wa utawala eneo hilo kuendeleza hamasa za mara kwa mara kwa wakaazi wa maeneo yao ili kutathmini changamoto zinazowakumba na kuzitatua mara moja.

“Naiambia kamati ya usalama eneo hili kutembea na kufanya baraza za usalama kuweza kuskia ile wananchi wanapitia kwa sababu wengi wanakosa usaidizi ndio watu wahalifu wakija wanaweza kuwapotosha”alisema Harrison.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Wakurugenzi wa Kampuni ya Bima ya Direct Line waagizwa kufika Mahakamani

Published

on

By

Mahakama ya Malindi imewaamuru wakurugenzi wa Kampuni ya Bima ya Direct Line kufika Mahakamani binafsi kwa ajili ya kuhojiwa.

Hii ni baada ya kampuni hiyo kushindwa kutekeleza amri ya Mahakama ya kulipa fidia ya shilingi milioni 2.26 kwa mwanamke aliyejeruhiwa vibaya katika ajali ya barabarani iliyokea Oktoba 6, mwaka 2016.

Kampuni hiyo, inayohusishwa na familia ya mfanyabiashara mashuhuri nchini ilishindwa kumlipa Hellen Waiyaki kiasi cha shilingi 2,259,825 kama ilivyoamriwa na Mahakama.

Waiyaki aliwasilisha kesi Mahakamani baada ya kampuni hiyo kukosa kutekeleza wajibu wake wa kulipa kiwango hicho cha pesa licha ya kuagizwa na Mahakama kufuatia ajali hiyo iliyohusisha basi la Tahir Sheikh Said Transporters Limited, maarufu kama TSS Bus Company, yenye nambari ya usajili KBZ 475S.

Akitoa uamuzi huo, Hakimu Mwandamizi wa Mahakama ya Malindi, Joy Wesonga, alisema ni lazima wakurugenzi hao wafike Mahakamani binafsi na kujieleza, akisema kampuni hiyo imekuwa ikiwazuia wananchi kufikia ofisi zao.

“Wakurugenzi hao watahitajika kufika mahakamani wakiwa na kuwasilisha vitabu vya hesabu vilivyokaguliwa vya kampuni, taarifa za benki pamoja na sajili ya mali za kampuni kwa kipindi cha miaka miwili ya mwisho ya kifedha ili Mahakama iweze kubaini uwezo wa kifedha wa kampuni hiyo na hali ya shughuli zake za kibiashara nchini Kenya.” alisema Hakimu Wesonga.

Katika hati kiapo kilichowasilishwa mahakamani kupitia wakili wake George Wakahiu, Hellen Waiyaki alisema alikuwa abiria ndani ya gari hilo ambalo lilikuwa likiendeshwa kwa uzembe kabla ya kupinduka na kusababisha ajali iliyomwacha na majeraha mabaya mwilini.

Kesi hiyo itaendeleza mnamo Julia 31 mwaka huu

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending