News
Kesi ya Mihadarati ya bilioni 8.2 kusikizwa Mahakama ya Mombasa
Kesi ya usafirishaji wa dawa za kulevya zenye thamani ya shilingi bilioni 8.2 iliendelea kusikilizwa katika mahakama ya Shanzu, shahidi wa pili ambaye ni afisa wa Jeshi la Wanamaji nchini akielezea mahakama kuwa jahazi lililokamatwa likiwa na dawa hizo halikuwa na utaifa wowote.
Akitoa ushahidi mbele ya Mahakama, Meja Mohamed Abdulrahman alisema chombo hicho kilikuwa kikifuatiliwa kwa muda mrefu na idara za kijasusi kutokana na tuhuma za usafirishaji wa mihadarati katika eneo la Afrika Mashariki na Pembe ya Afrika.
Kwa mujibu wa ushahidi, jahazi hilo lililojulikana kama MV Igor lilikamatwa umbali wa maili 350 kutoka pwani ya Mombasa likiwa halina bendera wala nyaraka zozote za usafirishaji.
Mahakama pia ilielezwa kwamba meli hiyo ilihusishwa na tukio la kushusha mzigo unaoshukiwa kuwa wa dawa za kulevya katika mji wa Maputo nchini Msumbiji mnamo Juni mwaka 2025.
Katika operesheni hiyo, maafisa wa wanamaji walikamata watu sita wanaodaiwa kuwa raia wa Iran na kupata bidhaa nyeupe inayoshukiwa kuwa dawa za kulevya ikiwa imehifadhiwa kwenye makasha madogo.
Vifaa vingine vilivyopatikana ni pamoja simu tano za rununu, simu ya setilaiti, kadi za utambulisho zenye maandishi ya Kiarabu pamoja na kadi za benki na laini kadhaa za simu.
Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa huku Mahakama ikitarajiwa kutembelea makao makuu ya Jeshi la Wanamaji kushuhudia vielelezo vilivyokamatwa.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

